Home » » KINANA AKERWA KUCHELEWA UJENZI WA BANDARI

KINANA AKERWA KUCHELEWA UJENZI WA BANDARI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Kinana akerwa kuchelewa ujenzi wa bandariCHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimeijia juu serikali kwa kumkumbatia mkandarasi asiye na uwezo wa kujenga bandari ndogo ya Karema, mkoani Katavi.

CCM imewaomba radhi wananchi wa Karema na Mkoa wa Katavi kwa jumla kutokana na madhara yanayosababishwa na kusimama kwa shughuli za uzalishaji na usafirishaji kupitia bandari hiyo.
Bandari hiyo imechelewa kwa zaidi ya miaka mitatu kwa sababu ya serikali kumkumbatia mkandarasi huyo.
Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Karema, Wilaya ya Karema, Mkoa wa Katavi, Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, alisema kitendo cha kuipa Kampuni ya Modispan kazi nne za ujenzi wa gati ambayo haina uwezo wa kuifanya ni cha kihuni kisichopaswa kufumbiwa macho.
Alisema serikali inapaswa kujieleza kwa nini mkandarasi huyo hadi leo hajanyang’anywa ukandarasi wa kujenga bandari hiyo licha ya kutokuwa na uwezo.
“Ndugu wananchi nakuombeni radhi kwa niaba ya CCM kutokana na kitendo hiki cha hovyo ilichofanyika, hatupaswi kujifanya hatuoni wakati mambo yako wazi kwa kazi kutofanyika.
“Yako maswali yanayopaswa kujibiwa kuhusu hiki kilichofanyika. Kwanza ni nani aliyempa mkandarasi huyu kazi ya ujenzi bila kujiridhisha na uwezo wake, pili kwa nini hadi sasa hajanyang’anywa kazi hii licha ya kubainika ameshindwa,” alisema.
Kwa mujibu wa Kinana, amelichukua suala hilo ili likajadiliwe  kwenye vikao vya juu zaidi na kumtafuta mchawi ili hatua zaidi zichukuliwe.
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kigoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa