Home » » MVUA ZWAKOSESHA MASOMO WANAFUNZI 450

MVUA ZWAKOSESHA MASOMO WANAFUNZI 450

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
ZAIDI ya wanafunzi 450 wa shule nne za msingi katika Kata ya Bumera, wilayani Tarime, watakosa masomo kwa muda usiojulikana kutokana na vyumba vya madarasa wanavyovitumia pamoja na nyumba za walimu kuezuliwa kwa upepo ulioambatana na mvua.
Mvua hiyo iliyonyesha Aprili 13, ilisababisha uharibifu katika shule za Kwisarara, Taisi, Kitenga na Kiterere zilizoathirika kwa kiasi kikubwa.
Katika Shule ya Msingi Kwisarara, vyumba viwili vya madarasa na ofisi ya walimu vimebomolewa kuta zake, huku nyumba ya mwalimu mkuu ikiezuliwa sehemu ya nyuma ya jengo hilo.
Akizungumzia athari hizo, mwalimu mkuu wa shule hiyo, Roche Rajab, alisema familia yake ilinusurika kifo kutokana na tufani iliyotangulia nusu saa kabla ya mvua kuanza kunyesha, ikizifanya kuta za nyumba kutikisika na kuwaogopesha watoto wake walioamua kukimbilia kabla  ya sehemu ya nyumba yake kung’olewa paa.
Shule ya Taisi yenye jumla ya wanafunzi 225, imelazimika kusimamisha masomo kutokana na madarasa yao kubomoka na sehemu ya paa na choo kuezuliwa na upepo.
Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Kitenga, Kandoro Kasoga, alisema amelazimika kulala katika nyumba ya wazi baada ya paa ya nyumba yake kuezuliwa na upepo.
 Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kigoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa