Home » » MBUNGE MACHALI ADAIWA KUMPIGABBA YAKE

MBUNGE MACHALI ADAIWA KUMPIGABBA YAKE

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

MBUNGE wa Kasulu Mjini, mkoani Kigoma, Bw. Moses Machali (NCCR-Mageuzi), anadaiwa kumpiga baba yake mzazi Mzee Joseph Machali kwa madai ya kutaka kumrekebisha tabia akidai kuchoshwa na kitendo chake cha kulewa pombe kupindukia.

Tukio hilo linadaiwa kutokea juzi ambapo mbunge huyo pia inadaiwa alimfukuza baba yake nyumbani na kumtupia nguo zake nje ambapo kutokana na kipigo hicho, Mzee huyo alikimbilia kwa mjumbe wa nyumba 10 aliyefahamika kwa jina la Dickson Joaqim.

Hatua hiyo imefuatia baada ya kuchoshwa na tabia hiyo na hivyo kuamua kumpatia kichapo hicho kwa lengo la kumrekebisha tabia jambo ambalo limesababisha kumpatia maumivu ya kutenguka kwa mkono.

Anadaiwa kuwa, siku ya tukio Mzee huyo alichelewa kurudi nyumbani na alipomgongea mwanaye (Mbunge Machali), alimfungulia na kuanza kumshushia kipigo hicho baada ya kuchoshwa na tabia yake.

Ili kuthibitisha madai hayo, Mwandishi wetu aliyepo mkoani Kigoma, alimpigia simu Bw. Machali ambaye alikiri kufanya tukio hilo na kudai kuwa, mzazi wake ana tabia ya kunywa pombe kupindukia hivyo kumuathiri yeye kisiasa anapowajibika kwa wananchi wake.

"Sikuwa na nia ya kufikia hatua ya kumpiga Mzee wangu, najitambua ndiyo maana namsihi aachane na pombe...najisikia vibaya kuona analewa, tukiwekana sawa, baadhi ya watu wanadai nampangia sheria," alisema.

Alisema kuanzia sasa, atakuwa sambamba na Mzee wake ambaye

baada ya kipigo hicho, alifungua kesi polisi lakini amekubali kuifuta na kwenda kulimaliza suala hilo kifamilia.

Baadhi ya wakazi wa eneo hilo, walidai kumuona Mzee huyo akiwa na fomu namba tatu ya matibabu inayotolewa na polisi (PF3) ambayo imemwezesha kupatiwa matibabu katika moja ya zahanati wilayani hapo.

Chumba cha habari Majira, kilifanya jitihada za kumpigia simu Bw. Machali ili aweze kuzungumzia tukio hilo kwa undani ambapo awali simu yake ilikuwa ikitumika na baadaye alizimwa kabisa.

Baada ya kumkosa Bw. Machali, Majira liliwasiliana kwa njia ya simu na Kamanda wa Polisi mkoani humo, Frasser Kashai ambaye alithibitisha jeshi hilo kupokea taarifa za Mzee Machali.

Alisema baada ya Mzee Machali kupeleka malalamiko ya kupigwa na mtoto wake, jeshi hilo lilifanikiwa kumkamata Bw. Machali na kumhoji ambapo jana ilikuwa apelekwe mahakamani kujibu mashtaka.

"Tukiwa kwenye harakati za kutaka kumpeleka mahakamani kwa tuhuma za kumpiga baba yake, mlalamikaji ambaye ni Mzee Machali aliomba kesi hii ifutwe ili wakalizungumzie suala hili nyumbani kifamilia," alisema

Chanzo:Majira

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kigoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa