Home » » WANAHABARI KIGOMA WATAKIWA KUJIUNGA MFUKO WA BIMA YA AFYA

WANAHABARI KIGOMA WATAKIWA KUJIUNGA MFUKO WA BIMA YA AFYA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
MENEJA wa Mfuko wa Bima ya afya Mkoa wa Kigoma (NHIF), Elias Odhiambo amewataka waandishi wa habari mkoani hapa kujiunga na bima ya afya ili kuondokana na hofu ya kukosa matibabu wanapoumwa.
Akizungumza na Waandishi wa Habari katika ofisi za Chama cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Kigoma (KGPC), Meneja huyo alisema kuwa, gharama ya kujiunga na mfuko huo kwa vikundi au taasisi isiyo ya serikali ni sh 76,300 kwa kila mwanachama, ambako atapata matibabu kwa mwaka mzima kwa fedha hiyo.
”Hivi sasa gharama za matibabu kwa kweli zipo juu sana, hivyo ni wakati wa kuangalia mnaelekea wapi, kujiunga na bima ya afya ni suala la msingi ili kuwa na uhakika wa matibabu unapougua, kwani unaweza kuugua kipindi ambacho huna hata pesa mfukoni, mtafakari vizuri na kufanya maamuzi,” alisema Odhiambo.
Meneja huyo alisema, huduma zinazotolewa na NHIF ni bora zaidi, kwani zinampa mwanachama uhuru wa kuchagua mahali au kituo anachopenda kupata huduma ya matibabu.
Alisema, hadi sasa NHIF imesajili vituo vya afya na maduka ya dawa 5,840 kwa nchi nzima, hali inayorahisisha upatikanaji wa huduma kwa wananchama.
Naye Mwenyekiti wa KGPC, Deogratius Nsokolo, alisema, wanachama wake watajiunga na mfuko huo kwa kuwa una manufaa makubwa na wataishawishi jamii kujiunga na mfuko huo.
Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kigoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa