Home » » UHAMIAJI KIGOMA YAHADHARISHA

UHAMIAJI KIGOMA YAHADHARISHA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Ofisa Uhamiaji wa Kigoma, Ambrose MwangukuIDARA ya Uhamiaji mkoa wa Kigoma imeelezwa wasiwasi wake wa nchi kuingia kwenye mtego wa kuchagua viongozi wasio raia kutokana na kuwepo madai ya viongozi wanaowahifadhi wahamiaji haramu na kuwaajiri.
Ofisa Uhamiaji wa mkoa, Ambrose Mwanguku aliyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari baada ya kupokea raia 14 waliomaliza kifungo cha mwaka mmoja gerezani kabla ya kurudishwa nchini kwao.
Alisema katika utendaji wa kazi zao, wamekuwa wakipata taabu kutoka kwa wananchi vijijini hasa viongozi wa vijiji ambao wamekuwa wakiwatumia raia hao wageni katika shuguli za uzalishaji mali hasa kilimo na uvuvi.
Mwanguku alisema kuwa baadhi ya wananchi wamekuwa wakitumia mbinu mbalimbali za kuhifadhi na kuwatumia raia wa kigeni bila ya kufuata taratibu na idara yake imekuwa ikipata taarifa juu ya kuwepo watu hao.
”Hali hii ya kuendelea kuishi katika jamii na raia wasio Watanzania inaweza hata kutupelekea kupata viongozi ambao si Watanzania, sasa kazi ya kutoa vitambulisho vya Taifa inakuja, kuna baadhi wanaweza kupata nafasi na kuandikishwa jambo ambalo ni hatari kwetu,”alisema.
 Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kigoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa