Home » » WATENDAJI WA SERIKALI,WANANCHI WAHIMIZWA KUSHIRIKIANA KULETA MAENDELEO

WATENDAJI WA SERIKALI,WANANCHI WAHIMIZWA KUSHIRIKIANA KULETA MAENDELEO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


 MKUU wa Wilaya ya Buhigwe mkoani Kigoma, Kanali Marco Gaguti akizungumza na Baadhi ya Watendaji wa Serikali na wananchi kushirikiana katika shughuli za maendeleo katika ukusanyaji wa mapato na kufanya kazi.
Na Rhoda Ezekiel Kigoma,

MKUU wa Wilaya ya Buhigwe mkoani Kigoma, Kanali Marco Gaguti amewataka watendaji wa Serikali na wananchi kushirikiana katika shughuli za maendeleo katika ukusanyaji wa mapato na kufanya kazi.
Lengo ni kuboresha huduma za kijamii katika Wilaya hiyo na kuinua uchumi wa wananchi na Taifa kwa ujumla.Mwito huo aliutoa juzi katika chakula cha pamoja na wazee wa Wilaya ya Buhigwe ,Watumishi wa serikali, viongozi wa dini na chama pamoja na kuhamasisha shughuli za maendeleo.
Ambapo aliwataka kila mwananchi mmoja mmoja, kwa makundi na kwa ujumla wao kuweka mikakati ya pamoja ya kusukuma mbele gurudumu la maendeleo ya elimu, afya, miundombinu na jinsi ya kupatikana haki za wazee.
Mkuu huyo aliwataka watendaji wa Halmashauri kwa kushirikiana na wananchi wote ndani ya Wilaya kusaidia jitihada za kusukuma gurudumu la maendeleo kwa kusimamia vizuri ukusanyaji wa mapato."Lengo ni kuwezesha upatikanaji wa huduma za kijamii kwa mafanikio makubwa ambapo mapato hayo yatasaidia vijiji ambavyo havina zahanati vipate huduma hiyo kutokana na mapato hayo," amesema.
Aidha Gaguti aliwataka watendaji wa Serikali kuhakikisha wazee wa Wilaya hiyo wanapata haki zao kama wengine ikiwa ni pamoja na kupatiwa matibabu bure, kwakuwa ni sera ya Taifa mzee asisumbuliwe na apatiwe huduma zote bila malipo.“Nawashukuru wazee, viongozi wa vya siasa, viongozi wa madhehebu ya dini na watumishi wote kwa kuonesha moyo wa kusimamia maendeleo yetu na kuhakikisha tunapata maendeleo kwa kasi."Ni imani yangu kuwa tutashilikiana kwa mambo mengi ili kuweza kuinua uchumi wetu", amesema Gaguti.
Katika hafla hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilya ya Buhigwe Anosta Nyamoga alieleza Halmashauri ya Buhigwe inatoa huduma za afya kwa wazee katika vituo vyake vya kutolea huduma za afya bure kulingana na sera na miongozo ya Serikali.
Aidha wazee wanapewa kipaumbele katika matibabu kwa kutibiwa kwanza. Pia wazee 14,993 wametambuliwa katika wilaya yetu na wazee 1000 watapigwa picha na kupewa vitambulisho vya matibabu katika kata 5.Upigaji wa picha na utoaji wa vitambulisho utaendelea katika kata 15 ambazo bado hazijafikiwa halmashauri imeendelea kuhamasisha jamii ili kuona umuhimu wa kujiunga na mfuko wa afya wa jamii (CHF). 
Nao baadhi ya wazee wa wilayani Buhigwe, Loleye Ndalibhonye alimpongeza Mkuu wa Wilaya kwa kuwakumbuka na kuwasaidia katika huduma za kijamii na kuwasaidia katika kuwapatia huduma ya afya bure.
Amesema endapo wilaya hiyo ikiongeza vituo vya afya itasaidia wazee hao kupata huduma kwa urahisi na Wananchi kuweza kupata huduma hiyo na kupunguza vifo vitokanavyo na ukosefu wa huda.
 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kigoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa