Home » » “UNYAMA KWA ALBINO KUATHIRI AMANI YA NCHI”

“UNYAMA KWA ALBINO KUATHIRI AMANI YA NCHI”

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

TUME ya Haki za Binadamu na Utawala Bora imeonya kuwa unyama unaofanywa kwa watu wenye ulemavu wa ngozi (albino), yatasababisha Tanzania kufutika kwenye ramani ya visiwa vya amani duniani.
Taarifa ya Kamishna wa Tume hiyo, Ali Hassan Rajab, imeeleza hayo na kuitaka Serikali na vyombo vyake vya dola, kuchunguza kwa kina waganga wa jadi, kutokana na madai kuwa ndio wanaochochea vitendo hivyo.
Rajab katika taarifa hiyo, alitoa mwito kwa Serikali na vyombo vya dola, kufanya uchunguzi wa kina kubaini wanaochochea, kufadhili na kutekeleza vitendo hivyo vya kinyama na kuwachukulia hatua kwa mujibu wa sheria.
“Kutokana na kuibuka tena kwa vitendo hivyo, ni dhahiri watu wenye ulemavu wa ngozi hivi sasa wanaishi kwa hofu na wanashindwa kufanya shughuli zao kwa uhuru, ikiwemo kujipatia riziki zao.
"Wanaporwa haki nyingine nyingi za binadamu kama haki ya kuishi, elimu na uhuru wa mtu kwenda atakako," ilieleza taarifa hiyo na kuitaka Serikali kutumia matokeo ya tafiti zilizokwishafanywa na wadau mbalimbali kupata ufumbuzi wa tatizo hilo.
Chanzo;Habari Leo

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kigoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa