Home » » WATUMISHI WA UMMA WATAKIWA KUBADILIKA

WATUMISHI WA UMMA WATAKIWA KUBADILIKA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

 Mganga Mkuu wa  Mkoa wa Kigoma Dkt. Paul Chote ambaye alikuwa mgeni rasmi wakati wa kufunga mafunzo kwa washiriki wa mafunzo ya mfumo wa kuandaa bajeti, mipango na kutoa ripoti (PlanRep iliyoboreshwa) kutoka mikoa ya Katavi, Rukwa na Kigoma akisisitiza  jambo kwa washiriki hao wakati akifunga mafunzo hayo.
Mmoja wa washiriki wa mafunzo hayo akizungumza muda mfupi kabla ya Hafla ya ufungaji mafunzo hayo iliyofanyika Mjini Kigoma. (Picha na Frank mvungi-Maelezo)

Frank Mvungi - Maelezo.

Serikali imewataka watumishi wa umma katika mikoa na Halmashuri kubadilika na kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia mabadililko ya mifumo yanayofanywa kwa kushirikina na wadau wa maendeleo.

Akizungumza wakati akifunga mafunzo ya mfumo wa kielektroniki utakaotumika kuandaa mipango,bajeti na kutoa ripoti yaliyowashirikisha washiriki kutoka Mikoa ya Katavi, Rukwa na kigoma, Mganga mkuu wa mkoa wa Kigoma ambaye alikuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo Dkt. Paul Chote amesema dhamira ya serika ni kuwawezesha watumishi wake kutekelza majukumu yao kwa ufanisi hasa katika kuwahudumia wananchi.

“Mfumo huu sio wa majaribio hivyo ni wajibu wa kila mshiriki kurudi katika mkoa na halmashuri na kuhakikisha kuwa anajenga uwezo kwa watumishi ambao hawakushiriki katika mafunzo haya kwa kuwa mfumo huu unahitaji uwajibikaji wa pamoja” alisisitiza Chote.

Akifafanua Dkt. Chote amesema kuwa washiriki wa mafunzo hayo wana jukumu kubwa lakutumia weledi na ujuzi waliopata kuleta mageuzi chanya katika maeneo yao ili azma ya serikali kutoa huduma bora itime. 

Kwa upande wake Muwakilishi kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI bw. Lisa Rwamiago amesema kuwa vituo zaidi ya elfu 22,000 vya kutolea huduma vitaunganishwa katika mfumo huo wa Kitaifa hali itakayofanya Tanzania kuwa nchi ya kwanza kusini mwa Afrika kwa kuwa na mifumo bora yakutolea huduma.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kigoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa