Home » » DAKTARI BINGWA WA MAGONJWA YA MOYO, STEPHAN P. MASATU KUENDESHA HUDUMA YA UCHUNGUZI WA MARADHI YA MOYO MKOANI KIGOMA

DAKTARI BINGWA WA MAGONJWA YA MOYO, STEPHAN P. MASATU KUENDESHA HUDUMA YA UCHUNGUZI WA MARADHI YA MOYO MKOANI KIGOMA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 DAKTARI bingwa wa magonjwa ya moyo, Dkt. Stephan P. Masatu

NA K-VIS MEDIA/Khalfan Said
WATU wanaosumbuliwa na maradhi ya Moyo mkoani Kigoma, watapata faraja kubwa mapema Aprili 4 hadi 9, 2016,  kufuatia uwepo wa huduma za uchunguzi wa maradhi hayo utakaofanywa na Daktari Bingwa wa magonjwa ya Moyo, Dkt. Stephan P. Masatu, kutoka jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi jijini Dar es Salaam, Dkt. Masatu alisema, huduma zote za magonjwa ya moyo ikiwa ni pamoja na vipimo vya ECG na ECHO  zitatolewa kuanzia asubuhi kwenye hospitali ya kibinafsi ya Upendo iliyo jirani na soko kuu la mkoani Kigoma.
Mkoa wa Kigoma ni miongoni mwa mikoa iliyo pembezoni mwa nchi na zinakabiliwa na upungufu wa wataalamu wa kushughulikia magonjwa kama ya Moyo na kutokana na uchache wa wataalamu hao, itakuwa ni nafasi nzuri kwa wananchi wa mkoa huo pamoja na vitongoji vyake, kujitokeza ili kuhudumiwa ambapo kliniki hiyo itadumu kwa muda wa siku sita mfululizo.


 Dkt. Masatu akitumia mashine ya kupima ECHO, mmoja wa wagonjwa wa moyo

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kigoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa