Home » » JESHI LA POLISI MKOANI KIGOMA LAFANIKIWA KUDHIBITI MOTO KATIKA MOJA YA MADUKA YA SOKO KUU MKOANI HUMO.

JESHI LA POLISI MKOANI KIGOMA LAFANIKIWA KUDHIBITI MOTO KATIKA MOJA YA MADUKA YA SOKO KUU MKOANI HUMO.




Baadhi ya raia wema na mmiliki wa duka Faustine Samweli wakishirikiana kuokoa mali ndani ya duka lililokuwa linaungua moto.
Freezer linalodhaniwa ndio chanzo cha moto huo.
Askari wa kikosi cha zimamoto manispaa ya Kigoma Ujiji wakiwa kwenye harakati za kuzima moto huo.
Wananchi wakishanga juhudi za polisi na zimamoto wakikabiliana na moto huo.
Na. Pardon Mbwate na Anamaria Masika wa Jeshi la Polisi Kigoma
Jeshi la Polisi mkoani Kigoma limefanikiwa  kuzuia na kuokoa  mali  na kudhiti moto kwa kushirikiana na askari zima Moto wa kikosi cha zimamoto Halmashauri ya Kigoma Ujiji na Kikosi cha zimamoto viwanja vya Ndege na baadhi ya vitu vimeokolewa na vingine kuungua bado thamani yake haijajulikana.
Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Kigoma SSP Kihenya Kihenya  amemtaja mmiliki wa duka hilo kuwa ni Faustine  Samweli 39, Mfanyabiashara wa Lumumba  Road chumba NO.16 kiliungua moto.
Kaimu Kamanda  amesema kuwa  Chanzo cha moto huo ni Freezer iliyokuwa imeachwa ikiwaka usiku mzima bila kuzimwa hivyo kusababisha chanzo cha moto huo.
Kamanda huyo amesema kuwa Thamani halisi ya mali iliyoteketea bado haijajulikana  na uchunguzi zaidi wa tukio hilo bado unaendelea.
Hata hivyo kamanda kihenya amewataka wafanya biashara wa eneo hilo kuhakikisha usalama wa mali zao kabla na baada ya kufanya shughuli zao kuwa waangalifu wakati wa ufungaji wa maduka yao ili kuzuia tukio la aina hiyo.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kigoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa