Home » » KATIBU MKUU WA UVCCM MARTIN SHIGELA ASHIRIKI SHUGHULI ZA KILIMO NA KUKAGUA MIRADI KIGOMA VIJIJINI

KATIBU MKUU WA UVCCM MARTIN SHIGELA ASHIRIKI SHUGHULI ZA KILIMO NA KUKAGUA MIRADI KIGOMA VIJIJINI



5 
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana CCM, UVCCM Bw. Martin Shigela akishiriki 
 katika kupalilia shamba la Karanga katika kijiji cha Nkungwe Tarafa ya 
Mabembe Wilaya ya Kigoma Vijijini wakati alipotembelea na kujionea shughuli 
mbalimbali na kukagua miradi inayotekelezwa na wananchi kwa pamoja na 
Serikali jana.
Sekretarieti ya CCM ikiongozwa na katibu mkuu wa CCM Ndugu Abdurahman 
Kinana  iko mkoani Kigoma kwa ajili ya  kuangalia utekelezaji wa Ilani ya Chama cha 
Mapinduzi na sherehe za miaka 36 ya chama hicho zinazotarajiwa kufanyika 
Februari 3 kwenye uwanja wa Lake Tanganyika mkoani humo, kulia ni Bi Fatma
 mmiliki wa na kushoto ni Khamis Bitese Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya 
Kigoma Vijijini.
3 Katibu Mkuu wa Umoja wa vijana CCM UVCCM Martin Shigela akisalimiana na wananchi wa kijiji cha Nkungwe wakati alipotembelea katika kijiji hicho jana
4 
Katibu Mkuu wa Umoja wa vijana CCM UVCCM Martin Shigela akikabidhiwa zawadi
 ya mihogo na Bi Asha Ibrahim mara baada ya kutembelea shamba lake jana, .
Kijiji hicho cha Nkungwe ndicho kinachoongoza kwa kilimo cha muhogo bra 
katika mkoa wa Kigoma.
8 
Katibu Mkuu wa Umoja wa vijana CCM UVCCM Martin Shigela akiongozana na
 Bw.Khamis Bitese Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kigoma Vijijini mbele yake 
wakati akikagua shughuli za ukulima wa kisasa katika kijiji cha Nkungwe Kigoma 
Vijijini, Kijiji hicho cha Nkungwe ndicho kinachoongoza kwa kilimo cha muhogo bra
katika mkoa wa Kigoma.
9 
Katibu Mkuu wa Umoja wa vijana CCM UVCCM Martin Shigela akimsaidia 
Bi. Asha Ibrahim kufukia mbegu ya Viazi, huku viongozi mbalimbali wa CCM  wilaya 
 ya Kigoma Vijijini wakishuhudia tukio hilo.
7 
Katibu Mkuu wa Umoja wa vijana CCM UVCCM Martin Shigela akimkabidhi 
 zawadi ya shilingi elfu 10,000 mtoto Rehema huku mama yake akimsaidia wakati 
alipotembelea na kujionea shughuli za kilimo katika kijiji cha Nkungwe jana
11 
Viongozi mbalimbali wakikagua kivuko cha Mto Ruchi katika kijiji cha 
Nkungwe jana.
12 
Katibu Mkuu wa Umoja wa vijana CCM UVCCM Martin Shigela akivuka katika 
kivuko cha Mto Ruchi kwa kutumia Baiskeli huku akiwa ameonozana na viongozi 
mbalimbali wa CCM wilaya ya Kigoma Vijijini pamoja na watendajiwa kijiji hicho 
jana inaelezwa kwamba watu wengi walipotea maisha kwa kuliwa na Mamba kabla 
ya kujengwa kivuko hiki.
13 
Katibu Mkuu wa Umoja wa vijana CCM UVCCM Martin Shigela akimenya 
muhogo
ili kutafuna kidogo mara baada ya kununua kwa mmoja wa wakulima Kijiji cha
 Nkungwe ndicho kinachoongoza kwa kilimo cha Muhogo mkoani Kigoma
15 
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana CCM UVCCM Martin Shigela akiagiza
 jambo kwa Mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa Kigoma Bw Peter Msanjila wakati 
alipotembelea kata ya Mwanduga jana kulia ni Khamis Bitese Mwenyekiti wa CCM
 Wilaya ya Kigoma Vijijini
16 
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana CCM UVCCM Martin Shigela akizungumza na
 wanafunzi wa shule ya msingi ya Kabanda katika kijiji cha Chabwimba jana
18 
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana CCM UVCCM Martin Shigela akisalimiana na
 wananchi mara baada ya kuwasili katika Kata ya  Mabembe.
19 
Wananchi wa kijiji cha Mabembe wakimsikiliza mwenyekiti wa UVCCM 
katika Kata ya Mabembe kwenye mkutano wa ndani
20 
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana CCM UVCCM Martin Shigela akicheza na 
msanii chipukizi wa kijiji cha Mabembe ambaye ni mlemavu wakati alipotembelea
 na katika Kata ya Mabembe
23 
Wananchi wakiwa wamejitokeza kwa wingi katika kata ya Mwanduga 
Kigoma vijijini jana
24 
Mjumbe wa NEC CCM kupitia Wilaya ya Uvinza Asha Baraka akiwa katika 
mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kata ya Mwanduga Kigoma jana kulia ni 
Khamis Bitese Mwenyekiti wa CCM Kigoma Vijijini na katikati ni Peter Msanjila Mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa Kigoma.
25 
Martin Shigela Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa akihutubia mkutano wa hadhara 
 uliofanyika jana kwenye kata ya Mwanduga Wilaya ya Kigoma vijijini
26 
Matin Shigela Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa akipata maeleo kutoka kwa 
Khamis Bitese Mwenyekitiwa CCM Wilaya ya Kigoma Vijijini  wakati alipotembele
 na kukagua ujenzi wa madarasa katika shule ya msingi ya Kabanda.
27 
Martin Shigela Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa akipata maeleo kutoka kwa 
Khamis Bitese Mwenyekitiwa CCM Wilaya ya Kigoma Vijijini  wakati alipotembele
 na kukagua ujenzi wa numba za walimu  katika shule ya msingi ya Kabanda.
2 
Huu ndiyo mto Ruchi unaotenganisha kijiji cha Nkungwe na mashamba ya 
wanakijiji hao uliosababisha mauaji ya wananchi kadhaa kutoka na kuliwa na 
Mamba kabla ya kujengwa kwa  kivuko hicho.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kigoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa