Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika
inakusudia kufuta mpango wa ruzuku ya mbolea ya pembejeo kwa wakulima
nchini kutokana na madai ya kukithiri kwa vitendo vya rushwa.
Kauli hiyo imetolewa hivi karibuni na Naibu Waziri
wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Godfrey Zambi alipokuwa katika ziara ya
wilaya za Kasulu na Uvinza mkoani Kigoma.
Akizungumza na vikundi vya wakulima (AMCOS), Zambi
alisema ruzuku hiyo itafutwa kutokana na vitendo vya rushwa ambavyo
hujitokeza wakati wa kuigawa katika misimu husika.
Aidha, alisema mpango wa kuanzisha benki ya
wakulima kwa ajili ya mikopo uko palepale ili kuwawezesha wakulima
kukopa na kuwajengea uwezo wa kumudu uendeshaji wa shughuli hiyo.
Alisema zaidi ya Sh74bilioni zimebainika kutumiwa
vibaya na watendaji wa serikali pamoja na mawakala wa pembejeo hizo
tangu kuanza kwa mfumo huo.
Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Uvinza, Khadija
Nyembo alisema licha ya mpango huo kuwa na lengo la kuwanufaisha
wakulima ulikabiliwa na changamoto mbalimbali kubwa ikiwa ni rushwa na
kwamba baadhi ya watendaji wa serikali wanatumikia vifungo gerezani.
Alisema wakulima wa Mkoa wa Kigoma wamekuwa
miongoni mwa waliokuwa wakilalamikia mpango huo kutokana na kuwanufaisha
wachache hivyo kutokuwa na tija katika kuboresha kilimo na uzalishaji.
Mkulima wa tumbaku huko Mwamila, Wilaya ya Uvinza,
Daniel Mkuyu alisema kuwa tatizo la rushwa katika ugawaji wa ruzuku ya
mbolea ya pembejeo limekuwa likijitokeza kila msimu wa kilimo na kwamba
dawa yake ni kuanzishwa kwa benki ya wakulima.
Chanzo Mwananchi
Chanzo Mwananchi
0 comments:
Post a Comment