Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Katibu
 Tawala wa Mkoa wa Kigoma, John Ndungulu akizungumza na waandishi wa 
habari kuhusu kusimamishwa kazi kwa watumishi 9 wa Manispaa ya 
Kigoma-Ujiji. (Picha na Emmanuel Senny).
Na Emmanuel Senny, Kigoma
Watumishi
 tisa wa Manispaa ya Kigoma-Ujiji wamesimamishwa kazi mara baada ya 
kubainika kuingia mikataba mibovu isiyokuwa na tija na kuisababishia 
manispaa hasara ya kupoteza mapato sambamba na kulipa fidia ambazo ni 
batili pamoja na kuuza mali za halmashauri kinyume cha sheria.
Maamuzi
 hayo yamefikiwa na ofisi ya Mkoa wa Kigoma baada ya Waziri Mkuu wa 
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, kubaini uuzwaji 
huo na kumuagiza Katibu Tawala wa Mkoa huu, kufanya uchunguzi wa awali 
kuhusu  tuhuma hizo ambapo alitakiwa kutoa mrejesho Januari 2 katika 
ofisi ya Waziri Mkuu.
Akizungumza
 na waandishi wa habari, Katibu Tawala wa Mkoa wa Kigoma, John Ndungulu,
 amesema, baada ya kuagizwa na Waziri Mkuu, aliunda kamati ya uchunguzi 
wa awali ambapo kabla ya Januari 2 walikuwa wameshakamilisha uchunguzi 
wa tuhuma hizo.
Alisema
 kuwa, awali tuhuma ambazo alizibaini Waziri Mkuu ni pamoja na uuzwaji 
wa majengo ya Manispaa likiwemo Jengo la Maendeleo ya Mkoa (KIGODEKO) 
lenye kiwanja namba 551 na Miboss lenye kiwanja namba 295 ambapo 
watuhumiwa walidai kuwa waliuza viwanja badala ya majengo.
“Tuhuma
 zingine zinazowakabiri watumishi hao ni manunuzi hewa ya vipuri vya 
gari SM 553 gari aina ya tipa vyenye gharama ya TSH. 8,002,000, Ununuzi 
hewa wa sajala yenye thamani ya Tshs. 4,640,000, matumizi mabovu ya 
fedha za serikali kwa ajiri ya matengenezo ya barabara yenye thamani ya 
Tsh. 18,000,000 kwa ajiri ya matengenezo na Tsh. 48,000,000 kwaajiri ya 
mkataba ambao haukufanyiwa kazi na matumizi yasiyoidhinishwa ya Tshs. 
809,633,407 ambazo zilitengwa kwaajiri ya miradi ya maendeleo badala 
yake zikapelekwa kwenye ujenzi wa maabara,” amesema Ndungulu.
Aidha
 Ndungulu amesema, uchunguzi wa awali uliofanywa na  kamati ulibaini 
kuwa watendaji wa manispaa waliingia mikataba mibovu isiyokuwa na tija 
na kuisababishia manispaa hasara ya kupoteza mapato sambamba na kulipa 
fidia ambazo ni batili, baadhi ya watendaji kushiriki katika ubadhilifu 
wa uuzwaji wa mali za manispaa bila kufuata utaratibu, ukodishaji wa 
jengo la KIGODEKO bila kufuata sheria.
Ndungulu
 amesema, baada ya kubainika kwa tuhuma hizo ofisi ya mkoa imeamua 
kuwasimamisha kazi watumishi hao ili kupisha uchunguzi zaidi kuhusu 
tuhuma hizo ambapo uchunguzi zaidi ukikamilika hatua zingine za kisheria
 zitafanyika.
Aliwataja
 majina watumishi waliosimamishwa kazi kuwa ni Wilfred Mwita (Mkuu wa 
Idara ya  Mipango  Manispaa), Emmanuel Mkwe (Mwanaseheria wa Manispaa), 
Mhandisi Boniface William (Mhandisi wa Manispaa), Mussa Igugu (Mkuu wa 
Kitengo cha Biashara), Elimboto Zacharia (Mkaguzi wa Ndani wa Manispaa),
 Leonard Nzirailunde (Afisa Misitu), Shida Thadei (Afisa Ugavi), Gwawili
 Mkoka (Mhasibu wa Manispaa) na Omary Hassan (Fundi Mkuu wa Magari).
Hata
 hivyo Ndungulu alisema, Ofisi ya Mkoa imemuagiza Mkurugenzi wa 
Halmashauri Mhandisi, Boniface Nyambele, kusimamia urejeshwaji wa mali 
za Manispaa zilizouzwa bila kufuata sheria na taratibu.
“Pia
 tumewaagiza jeshi la polisi na TAKUKURU kuchunguza tuhuma hizo kama 
kuna mianya ya rushwa ili kama kuwa watu walihusika katika utoaji wa 
rushwa basi nao washughulikiwe kwa mujibu wa sheria,” alisema Ndunguru.
0 comments:
Post a Comment