Na Jacquiline Mrisho - Kigoma 
Buluku
 aliongeza kuwa hadi sasa kuna jumla ya mashirika yasiyo ya kiserikali 
17 yanayoshirikiana na Serikali kuhudumia Kambi hiyo ambapo huduma zote 
zinaongozwa na Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR) hivyo, 
kazi kubwa ya Serikali ni kusimamia na kuhakikisha mashirika yote 
yanatoa huduma zinazofaa kwa wakimbizi hao. 
      
Serikali
 ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania imewasaidia jumla ya wakimbizi 
55,320 kutoka Burundi kwa kuwapa makazi na kuhakikisha ulinzi wa maisha 
yao katika Kambi ya Nduta iliyopo wilayani Kibondo, Mkoa wa Kigoma. 
Takwimu hizo zimetolewa na Mkuu wa Kambi  hiyo,
 Peter Buluku wakati akizungumza na mwandishi wa habari hii juu ya hali 
halisi ya maisha ya wakimbizi wanaoishi katika kambi hiyo pamoja na 
misaada inayotolewa na Serikali pamoja na Mashirika yasiyo ya 
kiserikali.
Buluku
 amesema kuwa wakimbizi hao ni raia wa Burundi ambao wamekimbia nchini 
kwao kutokana na vurugu zilizojitokeza mwezi Aprili mwaka 2015 ambazo 
zilisababisha raia hao kukimbilia nchi za jirani ikiwemo Tanzania.
“Sisi
 kama Serikali tunasaidia wakimbizi kwa kuwapa ardhi kwa ajili ya 
makazi, kuhakikisha ulinzi na usalama kwa wakimbizi,kupokea, kusajili na
 kutunza kumbukumbu za wakimbizi  pamoja na kuunganisha familia za wakimbizi zilizopoteana  wakati wa machafuko nchini mwao”, alisema Buluku.
Alifafanua
 kuwa kazi ya kutoa huduma za kijamii zikiwemo za Afya, Chakula, ujenzi 
wa nyumba, masoko,vyuo vya ufundi na miundombinu, Maji, huduma za haki 
za watoto na wazee wasiojiweza, elimu pamoja na huduma za kutoa misaada 
ya kisheria zinafanywa na mashirika yasiyo ya kiserikali yaliyojitolea 
kuwasaidia wakimbizi hao.
Mkuu
 huyo wa Kambi ametaja changamoto kubwa inayoikabili kambi hiyo kuwa ni 
upungufu wa rasilimali fedha kwa mashirika ambayo hali hiyo husababisha  baadhi ya shughuli za kuiwezesha kambi hiyo kutofanikiwa.
mwisho
0 comments:
Post a Comment