Home » » RAIS DKT MAGUFULI AMFAGILIA KAFULILA NYUMBANI KWAO

RAIS DKT MAGUFULI AMFAGILIA KAFULILA NYUMBANI KWAO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Na Editha Karlo- Globu ya Jamii Kigoma

RAIS Wa Jamuhuri wa Muungano Wa Tanzania Dkt John Magufuli amempongeza aliekuwa Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kusini ,David Kafulila kwa kujitoa Muhanga kutetea Watanzania kupitia sakata la Escrow(IPTL) na kuonesha uzalendo Mkubwa ambao hawezi kusahaulika katika historia ya Tanzania.

Akizungumza na Wananchi wa Kata ya Nguruka,leo Katika uzinduzi wa Mradi mkubwa wa Maji uliopo Tarafa ya Nguruka katika Wilayani Uvinza, alisema atakuwa mnafiki akishindwa kumpongeza Kafulila kwa kazi kubwa aliyoifanya ya kuibua Ubadhilifu uliofanywa na Kampuni ya IPTL ambapo kwasasa suala hilo ameanza kulifanyia kazi na mafanikio yameanza kuonekana.

Amesema Kafulila alitukanwa sana alipo ibua sakata la Escrow na kuitwa majina mengi ya kudhalilishwa kama tumbili na mengine mengi ya ajabu kwasababu ya uzalendo wake wa kutetea Taifa.

"Mimi ninafahamu unapoibua kitu cha kizalendo lazima usemwe, hivyo ninampongeza Kafulila kwa uzalendo wake kwa nchi na nitaendelea kumpongeza maisha yangu yote"alisema Magufuli.Magufuli alisema maendeleo hayana chama ndio maana Kafulila alijitoa kwa hali ya juu na kutetea fedha za Wananchi zilizo kuwa zikiibiwa na mafisadi wachache na kujinufaisha wao.

"Ninajua Kafulila ulitukanwa sana wakati wa kuibua sakata la Escrow, wapo watu walikuita tumbili mimi najua wewe sio tumbili ,matumbili ni wao wewe najua ni wa Chama kingine lakini umefanya kazi kubwa ya kulinda maslahi ya nchi, kwahiyo nitakuwa mnafiki sana nisipo kupongeza kitu ulichokifanya ni kikubwa Kwa,Taifa naomba nikupongeze kwa hilo",

Alisema Kiongozi mzuri ni yule ambae anatetea wananchi bila kujali chama wala siasa za uchochezi , hivyo atahakikisha kuwa Wananchi hawateseki na Wale ambao wameiba fedha za serikali na Wananchi wanazirudisha bila kujali nyadhifa walizonazo, ili pesa hizo zitumike katika kuleta maendeleo.

Rais Magufuli aliwaahidi Wananchi wa Nguruka atahakikisha anatatua kero ya Maji na umeme katika kata yao,kuhusu suala la umeme atamtuma Waziri wa Nishati na madini ili aweze kutatua tatizo hilo na kuwasaidia Wananchi kuepukana na shida hizo.

Rais Magufuli amemaliza ziara yake ya kikazi ya siku tatu Mkoani Kigoma kwa kuweka jiwe la msingi katika mradi wa Maji mkubwa katika kata ya Nguruka uliogharimu zaidi ya shilingi bilioni 2 ambao unatarajiwa kukamilika desemba 30 mwaka huu ambao utafuta kero ya maji kwa wananchi wa kata ya Nguruka.

Akiongea kwa njia ya simu na mtandao huu akiwa jijini Dar es Salaam aliyekuwa mbunge wa jimbo la Kigoma kusini kupitia tiketi ya chama cha NCCR Mageuzi David Kafulila kuhusu kauli ya Rais Kafulila amesema kuwa Rais amekuwa akimtia moyo kwani anaona kazi aliyokuwa akiifabya sasa imeanza kuleta matokeo mazuri.

"Kwakweli nafarijika na inanipa moyo wa kizalendo zaidi ninapo ona Rais anaunga mkono sakata la Escrow ambalo mimi ndo nililiibua wakati nikiwa mbunge japo nilipitia kwenye kipindi kigumu "alisema Kafulila

Kafulila alisema kuwa wakati akiwa mbunge kwenye sakata la Escrow msimamo wake na Rais ulikuwa unafanana toka bungeni

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kigoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa