Na Mwandishi wetu,KIGOMA.
Maafisa wa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu
(Idara ya Menejimenti ya Maafa) kwa kushirikiana na
Shirika la Kimataifa linaloshughulikia uhamaji (IOM) wameendesha
semina ya kujenga uelewa juu ya upunguzaji wa madhara ya
maafa katika jamii.
Mafunzo hayo yamefanyika tarehe 25 Machi 2025 katika
Manispaa ya Kigoma Ujiji ambapo yamehudhuriwa na
washiriki 50 ikiwemo Watendaji wa Kata, Watendaji wa
Vijiji, Watendaji wa Mtaa Kamati za Maafa za Kata na
Vijiji pamoja na mtaa.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa semina hiyo kwa
niaba ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma Ujiji Bi.Petronila Gwakila
ambaye ni Afisa Mazingira ndani ya Manispaa hiyo amesema,
mafunzo hayo yameletwa wakati sahihi ambapo manispaa
inatarajiwa kupata mvua ambazo mara nyingi mvua
hizo husababisha maafa mbalimbali na kufanya wananchi
kutofanya shughuli zao za kila siku za kuwapatia kipato hivyo
mafunzo haya yataweza kuleta muamko katika kukabili
maafa pindi yatakapotokea.
"Kwa hiyo ndugu zangu tumepata wakufunzi hawa juu ya
masuala ya Maafa ningependa sana tuwe makini kusikiliza
kutokana na kwamba hili jambo ni muhimu maana si mara
moja wala mara mbili maafa hasa ya mafuriko yanatukuta
sana katika maeneo yetu hata sasa mvua zimeshaanza na tumeanza
kuona athari zake hivyo tusikilize ili tujue namna ambavyo tunaweza
kujinusuru na jambo hili” amesema
0 comments:
Post a Comment