Home » » UKOSEFU WA VYOO KIGOMA, WAKAZI WAJISAIDIA KWENYE MIFUKO YA PLASTIKI NA KUITELEKEZA MITAANI

UKOSEFU WA VYOO KIGOMA, WAKAZI WAJISAIDIA KWENYE MIFUKO YA PLASTIKI NA KUITELEKEZA MITAANI

Na Diana Rubanguka, Kigoma Yetu

Wakazi wa Manispaa ya Kigoma Ujiji wako hatarini kupatwa na magonjwa ya mlipuko, kutokana na wakazi wake kuweka vinyesi kwenye mifuko ya plastiki na kuitupa mitaani kutokana na ukosefu wa vyoo.

Hayo yamebainishwa leo kwenye Mdahalo wa Mazingira ambao umekasimiwa na Asasi isiyokuwa ya Kiserikali ya Kigoma Un-Non Government Net-Work (KIUNGONET) ikiwa na lengo la kuwakutanisha asasi za kiraia na watendaji wa serikali kujadili changamoto ya uchafuzi wa mazingira ambayo imepelekea Manispaa ya kigoma Ujiji kutunukiwa hati chafu kwa kushindwa kudhibiti hali hiyo kwa miaka kumi huku mkurugenzi wa manispaa hiyo akkikacha kuhudhuria mdahalo huo.

Kakozi Abdallah mchangiaji alisema ,manispaa hiyo inakabiliwa na wakazi  wake  kuendelea kutumia mifuko ya Rambo kwa  kujisaidia haja kubwa na hatimaye huitelekeza mitaani,hali inayochochea kutokea kwa  magonjwa ya milipuko ,

Abdallah alidai kwamba, kutokana na hali tete ya uongozi wa halmashauri ya Kigoma ujiji kushindwa kuwa na magari ya maji machafu pamoja na kushindwa kudhibiti jamii husika na sheria ndogo ndogo ni chachu ya manispaa hiyo kushiriki kuchafua mazingira kwa 60%.

Hellena Geogre ni miongoni mwa wadau wa usafi wa mazingira alisema kuwa,jamii haina elimu juu ya mabadiliko ya tabia nchi kuwa ni pamoja na utupaji wa taka hovyo,hivyo kupitia midahalo ya asasi za kiraia wanachi waelimishwe ili kudhibiti vitendo vya utupaji wa vinyesi holela.

“ ikiwa viongozi wa serikali hawataki kuja kwenye mdahalo kama huu wa kujadili pamoja nini kifanyike na changamoto ya uchafunzi wa mazingira,watu wataendelea kujisaidia ziwani na vinyesi vitatupwa sana tu,”alisema Mh,Diwani Kata ya Buzebazeba Maftah.

Juma Ramadhan  Katibu Meza ya Duara alisema kuwa,tija iliyopo ni ushirikiano kwa asasi zote za kiraia Kigoma kuhamasisha jamii kupitia mikutano na semina kuwa jamii, ibadilike na tabia za uchafu,  kwani mazingira safi ni pamoja na afya njema.

Naye Mkurugenzi wa KIUNGONET Costasine Mosha alisema kwamba,wenyeviti wa Serikali za mitaa hawana elimu sahihi ya usafi wa mazingira na wajibu katika mitaa yao,hali inayochangia jamii kujenga utamaduni wa kujisaidia ziwani badala ya vyoo,wakidai “kujisaidia ziwani kuna raha yake”.

Blogzamikoa

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kigoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa