Na Mwandishi Wetu, Kigoma Yetu.
Mahakama ya hakimu mkazi Mkoa
Kigoma imewahuku kifungo cha miezi sita mahabusu watatu wanaotuhumiwa kwa
makosa ya mauaji kufuatia kitendo cha kufanya fujo mahakamani wakilalamika kesi
yao kuchukuliwa muda mrefu bila kutolewa hukumu.
Mahabusu waliohukumiwa kifungo
hicho na Hakimu mkazi mkoa kigoma Emanuel Mrangu ni Maneno Kichako, Majuto
Dunia na Haruni Petro ambao inaelezwa kuwa waliongoza mgomo na kufanya fujo
mahakamani hapo wakishinikiza mgomo wa mahabusu kugoma kuingia mahakamani.
Mrangu aliwahukumu kifungo
hicho cha miezi sita jela watuhumiwa hao kwa kosa la kufanya fujo mahakamani na
kusema kuwa kama walikuwa na madai yao kuhusu kucheleweshwa kwa mwenendo wa
kesi zao walipaswa wapeleke malalamiko hayo kwa kufuata taratibu za kimahakama
lakini si kufanya fujo mahakamani na hivyo kesi mbalimbali zilizokuwa
zikiendeshwa kusimama kwa muda.
Awali mashuhuda wa tukio hilo
walieleza kuwa mara baada ya karandinga la polisi lilipowasili mahakamani hapo
mahabusu hao waligoma kushuka na badala yake walianza kupiga kelele huku
wakifunga mlango wa kutokea katika gari hilo ili kuzuia polisi kushindwa
kuwashusha.
Hali hiyo iliwalazimu askari
walioongozana na gari hilo kulipeleka gari hilo kituuo kikuu cha polisi mjini
Kigoma na hapo walianza kupewa kipigo ili kuwafanya kulainika na kuruhusu
ratiba ya siku kuendelea.
Aidha kwa mujibu wa mashuhuda
hao walieleza kuwa katika sarakasi hizo mahabusu mmoja aliumia kwa kile
kinachoelezwa kuwa kizidiwa na kipigo kutoka kwa askari polisi na hivyo
kukimbizwa hospitali ya mkoa Kigoma Maweni kwa matibabu.
Kamanda wa polisi mkoa kigoma
alikiri kutokea kwa mgomo huo wa mahabu na kusema kuwa ni hali ya kawaida
lakini tatizo hilo liliisha katika muda mfupi ambapo alikana kuumizwa kwa
mahabusu huyo kwa kipigo cha polisi badala yake alisema kuwa mahabusu huyo
alianguka kutoka kwenye gari na kuumia.
Aidha Hakimu mkazi
mfawidhi mkoa kigoma, Emanuel Mrangu alikiri kuwepo kwa vurugu hizo na
kusema kuwa waliohusika na vurugu hizo walikuwa ni mahabusu watatu ambao
wanakabiliwa na kesi ya mauaji ambao wanalalamika kesi yao kuchukua muda mrefu
bila kwisha.
Hata hivyo alisema kuwa
amewasiliana na uongozi wa magereza mkoa Kigoma kuona namna gani suala kama
hilo linapatiwa ufumbuzi ikiwemo suala la mchakato wa kesi kuchukua muda mrefu
huku akitoa angalizo la kuwataka maafisa magereza kuandika barua za maombi wa
mwenenndo wa kesi kukumbusha kushughulikiwa kwa kesi ambazo zimechukua muda
mrefu bila kumalizika.
Jopo la waandishi wa habari
lilitembelea pia hospitali ya mkoa kigoma Maweni na kupata taarifa za mahabusu
aliyelazwa hospitalini hapo aliyefahamika kwa jina la maneno Kichako ambapo
viongozi waandamizi hospitalini hapo waliakataa kutoa ushirikiano kwa waandishi
wa habari kuhusu kuwepo kwa mahabausu huyo hospitalini hapo.
Aidha waandishi walifanikiwa
kupata uthibitisho kutoka kwa mtumishi mmoja wa hospitali hiyo alieleza kuwa
mahabusu huyo kwa sasa yuko Wodi namba saba lakini hakuna mwandishi yeyote
ambaye anaruhusiwa kuingia wodini humo kwa sasa.
Blogzamikoa
0 comments:
Post a Comment