na Betty Kangonga
KAIMU
Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika, Sophia Kaduma, amesema
Siku ya Chakula Duniani mwaka huu kitaifa itafanyika mkoani Kigoma katika
kijiji cha Kalinzi.
Katika
taarifa kwa vyombo vya habari jana, Kaduma alisema Watanzania wataungana na
wanachama wa Umoja wa Mataifa katika kuienzi siku hiyo iliyoanza jana na
kufikia kilele Oktoba 16 mwaka huu kwa kutambua mchango na umuhimu wa chakula
katika jamii.
Alisema
kaulimbiu ya mwaka huu ni “Ushirika katika kilimo: Ufunguo wa kulisha dunia”
ambayo inalenga kuonyesha umuhimu na nafasi ya ushirika katika kuzalisha
chakula kwa ajili ya kutosheleza mahitaji ya watu wote na kwingineko duniani.
Alisema
sherehe hizo zitafunguliwa na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Issa Machibya, na
kufungwa na Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika, Christopher Chiza.
Kaduma
alisema sherehe hizo zinatilia maanani umuhimu wa chakula na nafasi yake kwa
jamii kwa kuonyesha mafanikio na changamoto za upatikanaji wake kuanzia ngazi
ya kijiji hadi taifa.
Alisema
maadhimisho hayo yataenda sambamba na maonesho ya wadau wa kilimo na chakula
vikiwemo vikundi vya wajasiriamali, wakulima, wavuvi, wafugaji na sekta
binafsi.
Chanzo: Tanzania Daima
0 comments:
Post a Comment