Home » » Auawa akiiba mabati JKT

Auawa akiiba mabati JKT



na Mwemezi Muhingo, Kibondo
MKAZI wa Kijiji cha Kaziramihuda, Wilaya ya Kakonko, Mkoa wa Kigoma, Mohozya Joakimu (25), ameuawa kwa kupigwa risasi huku wengine saba wakikimbilia kusikojulikana baada ya kukutwa wakiiba mabati katika kikosi 824 cha Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Kanembwa.
Taarifa kutoka eneo la tukio zilisema kuwa, Joakimu akiwa na wenzake nane, walikutwa juu ya paa la jengo moja wakiezua mabati ndani ya kikosi hicho, ndipo askari waliokuwa doria waliwabaini na kupiga risasi iliyompata mtu huyo.
Tukio hilo limetokea Novemba 19, mwaka huu, saa 6:00 usiku katika Kikosi cha 824 KJ, Kanembwa, Wilaya mpya ya Kakonko.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma, Freiser Kashai, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuwataka wananchi kuacha tabia za uharibifu wa mali za umma.
Eneo hilo kabla ya kuchukuliwa na JKT lilikuwa likitumiwa kama kambi ya kuhifadhi wakimbizi wa Burundi waliokimbia vita mwaka 1994.


0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kigoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa