Na, Mwandishi Wetu, Kigoma.
Mkuu
wa gereza la Bangwe lililopo manispaa ya Kigoma Ujiji, SSP Raphael
Mwanyingili ameupongeza Mradi wa hifadhi wa Bonde la Ziwa Tanganyika kwa
kuwajengea wafungwa majiko banifu ya kuni tatu ambayo hupunguza kasi ya ukataji
wa miti kutokana na majiko hayo yanayobana matumizi ya kuni pamoja na kupunguza
moshi ambao huathiri watumiaji wa nishati hiyo.
Pongezi hizo zimetolewa mkoani hapo wakati wa mkutano wa
kamati ya dharura iliyokuwa ikiwajibika kuboresha mapungufu ya makala ya Mradi
wa hifadhi bonde la ziwa Tanganyika ambao ulifanywa na jopo la waandishi wa
habari kutoka kanda ya ziwa ikiwa na lengo la kuelezea utendaji kazi wa
mradi huo pamoja na matokeo yake kwa vijiji tarajiwa sita ambavyo vimefanikiwa
kupewa uwezo na mafunzo juu ya kulinda vyanzo vya maji na kuhifadhi
mazingira kutokana na matumizi ya jiko banifu.
Aidha SSP Raphael Mwanyingili alisema
kuwa, mradi wa hifadhi bonde la ziwa Tanganyika imeonesha dhati ya kupunguza
kero ya ukataji miti kwa kusudi la nishati ya moto katika vijiji teule
ilagaga,kibondo,katavi,rukwa ,kasulu na kigoma pamoja na kuzisaidia tasisi za
kiserikali likwemo gereza la bangwe hali iliyopunguza matumizi ya kuni
nyingi kutoka tani qubiki 15 hadi tani 5 qubiki kwa mwezi.
“ sisis tunakata kuni kutoka msitu wa
kutengenezwa tumeupanda upo karibu na gereza hatua kumi na tano tu, hili
gereza linahifadhi wafungwa na mahabusu si chini ya 3,000
hivyo kiasi cha kuni kinahitajika kwa wingi lakini kupitia mradi wa Bonde
la ziwa Tanganyika imeisaidia serikali kupunguza fedha za kununua miche ya
kurudishia miti ya m situ” alisema Mwanyingili.
Kwa upande wake Meneja mradi wa Bonde hilo Selebon Mushi,
alisema kuwa dhamira ya mradi ni kuwaweka
wananchi katika utayari wa kupokea mabadiliko ya tabia nchi iwe
fursa kwa vijiji darasa wabadilishe kilimo cha kuhamahama ,tumbaku na
matumizi ya mbolea kwa kufuga nyuki ambayo ina tija kwa familia zao na rafiki
wa mazingira.
Naye Leonard Nzilayilunde Afisa Mazingira
Manispaa ya kigoma alisema kuwa, mradi umebaini manispaa ya kigoma ujiji kukosa
eneo maalum la kutupa taka ngumu hali inayochochea wananchi kutupa taka holela
na kusababisha uchafuzi wa ziwa hilo hali inayokwamishwa na miundombinu duni ya
kuhifadhi taka hizo,huku akidai changamoto hiyo itakwisha mwaka huu baada ya
kukamilika kwa ujenzi wa `Landfield ambapo taka hizo ambazo zitakuwa ajira kwa
vijana pindi litakapokamilika.
0 comments:
Post a Comment