Home » » Mamlaka ya Ziwa Tanganyika yatoa vitabu vye elimu ya mabadiliko ya tabianchi

Mamlaka ya Ziwa Tanganyika yatoa vitabu vye elimu ya mabadiliko ya tabianchi


Na Mwandishi Wetu, Kigoma.
Mkurugenzi Mtendaji Mamlaka ya  Ziwa Tanganyika  kutoka Burundi  Kaitira Katonda amekabidhi  vitabu vya mpango mkakati wa kulinda na kuhifadhi ziwa Tanganyika  kwa mradi wa  Programu  shirikishi ya Usimamizi wa ziwa Tanganyika kwa dhumuni la kuwafanya wadau wa ziwa hilo kubaini mabadiliko ya tabia nchi kwa fursa ya kulinda na kuhifadhi ziwa hilo.
Akikabidhi vitabu hivyo Mbele ya Mkuu wa Wilaya ambaye ni mgeni lasmi kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma  Lt.Mstaafu Issa Machibya, alipokea vitabu hivyo kwa niaba ya  Lt.Machibya sambamba na fulana ,beji na kofia ambazo  zina rangi za nchi Nne  ambazo ni Congo DRC Zambia, Tanzania na Burundi ikiwa na hamasa ya uzalendo kwa viongozi husika ili iwe  utambulisho wao pindi wanapokuwa katika majukumu ya utekelezaji wa mradi .
Katonda alisema kuwa, kutokana na changamoto ya ziwa hilo ambalo linatumiwa na nchi hizo, hawana budi kuwaelimisha wananchi juu  ya lengo la kuendeleza shughuli zao za uvuvi,kilimo,hifadhi za wanyama na mimea, ili iwe chachu ya kuenzi ziwa hilo kwa kizazi kijacho bila kuathiri viumbe hai waishio ndani ya ziwa hilo hali itakayosaidia ziwa hilo kupungua kwa joto kutokana na changamoto ya  ziwa hilo kuongezeka kwa joto hali inayohatarisha uhai wa viumbe hai.  
Kwa Upande wake mgeni rasmi  ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya  kwa niaba ya mkuu wa mkoa Ramadhan Maneno alisema kuwa, amebaini tija ya kuzindua vitabu hivyo ambavyo ni chachu  kwa wananchi tegemezi wa mazao ya ziwa hilo kukubali mabadiliko kulingana na karne ili ziwa liwe endelevu kwa jamii husika siku zijazo  huku akizitaka halmashauri za manispaa za mjini na wilayani kwa lengo la kubaini ubadhirifu wa ziwa hilo kwa sheria na kanuni husika za mazingira.
“nazindua rasmi matumizi ya hivi vitabu, beji, kofia na fulana hii ni tija kwa wahusika wawajibike kulingana na hali halisi ya jamii yake lengo ziwa liwe salama na endelevu kwa wajukuu zetu,bila kuisahau ofisi ya makamu wa raisi mazingira katika jitihada zake za kuwainua wadau wenye kuelimisha wananchi juu ya mabadiliko ya nchi na fursa kwa kuhifadhi na kulinda misitu,uoto wa asili kwa njia mbadala ya uvunaji wa mazao ndani ya ziwa” alibainisha Maneno.
Naye Meneja Mradi Magese Bulayi alitoa wito kwa asasi za kiraia ambao wanahitaji kushiriki kwenye shughuli za uhifadhi wa mazingira wasisite kwenda kwenye  mradi wao ili wapatiwe malengo sita mtambukwa ya kuzingatia pindi wanapoelimisha wananchi ili kuokoa uchafuzi wa mazingira ambayo ni chachu kwa kuathiri viumbe hai siku za usoni.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kigoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa