Home » » KIZIMBANI KWA KUKAMATWA NA NYAMA YA TEMBO

KIZIMBANI KWA KUKAMATWA NA NYAMA YA TEMBO

Na, Diana Rubanguka, Kigoma.
JESHI la Polisi Mkoani Kigoma limemfikisha mahakamani Mathayo Ndolibihundo (30) Muha na Mkurima wa Nengo Wilayani Kibondo kujibu shitaka la kukamatwa na Nyama ya Tembo kilo 15 zenye thamani ya zaidi ya 2m Tsh.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kamanda wa Polisi Mkoani Kigoma ACP Fraisser Kashai amesema kuwa mnamo 16 April 2013 majira ya saa 9:45 katika kijiji cha Kabanga kilichopo Wilaya ya Kibondo mkoani humo, askari polisi wakiwa doria walimkamta mtuhumiwa huyo na kumfikisha kituoni.
Wakati huo huo, Jeshi la Polisi Mkoani humo linawashikilia watu wawili Abasi Kalaheze (58) muha na mkulima wa kijiji cha Sogeeni kilichopo wilayani Ksulu na Tashimililo  Ejide ambaye ni raia wa nchi jirani Burundi (Mhutu) (25) kwa tuhuma za kukamtwa na miche ya Bhangi.
ACP Kashai alisema kuwa watuhumiwa hao walikamatwa na askari polisi wakiwa kazini mnamo 17 April 2013 majira ya saa 12:00 katika kijiji cha Sogeeni Tarafa ya Heru chini iliyopo wilayani Kasulu Mkoani Humo wakiwa wamepanda miche 30 ya bhangi shambani kwa kuichanganya na tumbaku.
Aidha kashai alisema kuwa watuhumiwa wamefikishwa mahakani leo ili kijibu mashitaka yanayowakabili, pia ametoa wito kwa wananchi kuendelea kushirikiana na polisi ili kufichua uharifu na waharifu.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kigoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa