Home » » Mafuriko yaua Kigoma

Mafuriko yaua Kigoma

Na Diana Rubanguka, Kigoma.

WATU wanne Mkoani Kigoma wamekufa  katika matukio tofauti likiwemo la watu wawili kusombwa na mafuriko sambamba na kaya 200  wakati  zaidi ya hekari 2000 kuharibiwa na mafuriko hayo  yaliyotokea katika Kijiji cha Mgambazi eneo la mwambao wa Ziwa Tanganyika katika Wilaya ya Uvinza Mkoani Kigoma.

Akitoa taarifa hiyo leo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma Frasser Kashai  alisema kuwa tukio la kwanza lilitokea Aprili 11 mwaka huu  saa 9.usiku   ambapo chanzo cha mto huo kujaa ni mvua kubwa iliyonyesha milimani kwenye kijiji cha mshamu mpakani na mpanda ambapo ulisababisha mto  Mgambazi uliopo katika Kijiji hicho kujaa na kusababisha madhara hayo kwa wananchi wa eneo hilo.

Akiwataja marehemu hao waliosobwa na mafuriko hayo Kamanda Kashai  alisema ni  Tabu Lubayi (25) na Nyamwelu Rashid (22) wote wakazi wa Kijiji cha Mgambazi katika Wilaya ya Uvinza Mkoa wa Kigoma ambapo tukio hilo lilitokana na mvua kubwa iliyonyesha kutwa nzima na kusababisha mto Mgambazi kujaa maji na kuingia katika mashamba na nyumba za watu hao.

Aidha Mwenyekiti wa ulinzi na Usalama  Mkuu wa Mkoa Kigoma Lt. Issa Machibya aliwataka wakazi wa eneo hilo kuhama haraka iwezekanavyo ili kuepuka na madhara mengine yanayoweza kujitokeza kwa kipindi hiki cha masika.

Katika tukio hilo  mwili wa mtu mmoja ulipatikana katika eneo la mtoni huku mwingine kutoonekana hadi sasa na taratibu za kuutafuta zinaendelea ambapo taarifa mbalimbali zinaeleza kuwa mafuriko kama hayo yalishawahi kutokea miaka mwaka 1999 na kusababisha madhara na kuziomba asasi mbalimbali zishiriki kuzisaidia wahanga hao kimalazi,chakula na mavazi.

Katika tukio lingine lililotokea aprili 14 mwaka huu, majira ya saa tisa usiku katika Kijiji cha Kasuga Wilaya ya Kakonko Mkoa wa Kigoma watu wasio julikana walivamia nyumba ya mkazi mmoja na kufanya mauwaji pamoja na kujeruhi mtoto wa miaka sita.

Kamanda Kashai alimtaja bw. Nyamwelu Nesteli (30) ambaye alivamiwa na watu hao na kupigwa risasi maeneo ya kifuani na kumsababishia kifo chake hapo papo pamoja na kumjeruhi mtoto wa marehemu katika eneo la mkono wa kushoto ambaye alikuwa amelala ndani.

Aidha katika tukio lingine lililotokea Aprili 14 mwaka huu majira ya saa moja jioni katika eneo la Reli Mpya Kata na Tarafa ya Nguruka Wilaya ya Uvinza Mkoa wa Kigoma Abel Chikobela (65) aliuwawa kwa kupigwa na kitu kizito eneo la kichwani kutokana na ugomvi wa kugombania miradhi.

Kamanda Kashai alimtaja aliyehusika na mauaji hayo kuwa ni Ntauma Abel (31) mkulima na mkazi wa Nguruka alimuuwa ndugu yake kwa ajili ya kugombania miradhi waliyoachiwa na wazazi wao, ambapo mtuhumiwa yupo chini ya ulinzi wa polisi na anatarajiwa kufikishwa mahakamani baada ya upelelezi kukamilika.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kigoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa