Home » » POLISI KIGOMA YAENDESHA MSAKO MKALI KUKAMATA MAJAMBAZI SITA WALIOVAMIA NA KUPORA KATIKA SHULE YA RUNGWE.

POLISI KIGOMA YAENDESHA MSAKO MKALI KUKAMATA MAJAMBAZI SITA WALIOVAMIA NA KUPORA KATIKA SHULE YA RUNGWE.

Na Diana Rubanguka, Kigoma.
Jeshi la Polisi Mkoani Kigoma linawasaka watu sita wanaodhaniwa kuwa ni majambazi kwa tuhuma za kuvamia Shule ya Sekondari ya kutwa ya Rungwe Mpya iliyopo wilaya ya Kasulu Mkoani humo.
Tukio hili lilotokea 21 April 2013 majira ya saa 01:00 usiku limethibitishwa na Kamanda wa Polisi Mkoani Kigoma ACP Fraisser Kashai  ambapo alisema kuwa watuhumiwa hao walimfunga kamba Mlinzi wa Shule hiyo Obedi Muhindi (45) Mkazi wa  Rungwe  Mpya na kupora Solar Panel 05, Invetor 01, Simu tatu za mkononi, Laptop 01 pamoja na pesa taslim kiasi cha Tsh 45 elfu.
ACP Kashai alisema kuwa Majambazi hao walipanda juu ya paa za madarasa na kuzingoa Solar hizo na kutokomea nazo.
Aidha alisema kuwa Majambazi hao walimkatakata Mlinzi huyo kwa mapanga sehemu mbali mbali za mwili wake na amelazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Kasulu kwa matibabu.
Hata hivyo  alisema kuwa kufuatia msako mkali uliofanyika kwa kushirikiana na wananchi Soral zote zilizokuwa zimeporwa zilikutwa zimetelekezwa Porini na baada ya waharifu hao kuwaona Polisi na wananchi wakiwafuatilia.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kigoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa