Home » » Wahanga wa mafuriko ya mwezi Aprili wapewa msaada

Wahanga wa mafuriko ya mwezi Aprili wapewa msaada

Na Diana Rubanguka, Kigoma
Idara ya Maafa Ofisi Ya Waziri Mkuu imetoa msaada wa vifaa vya kujikimu  kwa Wahanga wa mafuriko yaliyotokea Aprili 11 katika kijiji cha Mgambazi kata ya Igalula wilayani Kigoma.
Vifaa hivyo vimetolewa jana katika Kijiji hicho chini ya  Mratibu wa maafa Mkoa wa Kigoma bw. Rashid Maftaha ambapo amesema kuwa chanzo cha mafuriko hayo ni baada ya mvua kali kunyesha na kusababisha Mto Mgambazi kujaa na hivyo kusababisha vifo  vya watu wawili na zaidi ya wakazi 500 kupoteza makazi yao.
Akikabidhi vifaa hivyo Mratibu huyo alisema  kuwa vifaa hivyo vimegharama kiasi cha  jumla ya shilling Milioni saba ikiwa ni pamoja na mahema, branket, sufuria na mafuta ya kupikia.
Kwa upande wake Kaimu Mtendaji Kata ya Igalula Kijiji cha Mgambazi bw. Oscar Cosmas ametoa shukrani na kuomba misaada hiyo iweze kuwa endelevu ili kuwanusuru wakazi hao.
Aidha tukio hilo la mafuriko katika kijiji hicho ni la mara ya pili awali tukio hilo lilitokea mwaka 1999 ambapo kijiji hicho ni miongoni mwa vijiji ambavyo vinakabiliwa na ukosefu wa mawasiliano na hivyo taarifa za mafuriko kuchukua zaidi ya siku 5 kuifikia serikali ya mkoa wa Kigoma.
Hata hivyo wakazi wa kijiji hicho wameiomba serikali kuweka mitambo itakayo wezesha mawasiliano kufuatia matatizo hayoambayo yamekua yakiwakumba.


0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kigoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa