Home » » Watalii waongezeka hifadhi ya Gombe

Watalii waongezeka hifadhi ya Gombe


BAADA ya serikali kupitia wizara ya maliasili na utalii kujitangaza kwenye mipaka yake ya ndani na nje ya Tanzania hatua hiyo imeanza kuonyesha mafanikio kutokana na ongezeko la idaidi ya watalii wanaokuja nchini kwa ajili ya kutazama vivutio mbalimbali.

Miongoni mwa vivtutio hivyo ni hifadhi za taifa, mapori tengefu, maporomoko ya asili, mila na tamaduni za maisha ya waafrika na mlima Kilimanjaro ambavyo kwa pamoja vimeifanya Tanzania kujulikana kimataifa.


Hifadhi ya Gombe ipo umbali wa km 16 kaskazini  mwa mji wa kigoma, katika fukwe za ziwa Tanganyika Magharibi mwa Tanzania ambako anapatikana Sokwemtu mnyama mwenye mila, desturi na tamaduni kama za binadamu ikiwemo kumiliki familia na kuwa na ukoo.

Kama ilivyo kwa binadamu sokwemtu ana uwezo wa kuishi zaidi ya miaka 50 hatua ambayo imekuwa kivutio kwa watalii wa ndani na nje ya nchi kutumia pesa nyingi katika kusafiri ili kujionea uhalisia huo.

Mhifadhi mkuu wa hifadhi Bi. Noelia Myonga amesema fursa hiyo ya kutangaza maliasili na vivutio imeiwezesha hifadhi ya taifa Gombe iliyopo mkoani Kigoma kuwa na ongezeko la watalii kutoka 130 kwa mwaka 2008 hadi kufikia 2500 Juni mwaka huu.

Kabla ya kutangazwa kuwa hifadhi ya taifa mwaka 1968, hifadhi ya taifa Gombe ilikuwa ni pori tengefu ambalo lilitumiwa na mwingereza Jane Goodall kwa masuala ya utafiti wa maisha ya Sokwemtu kupitia taasisi aliyoipa jina lake.

ENDELEA KUSOMA HAPA>>>

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kigoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa