Home » » Ufisadi wanukia ujenzi wa bandari mpya ya Kibirizi

Ufisadi wanukia ujenzi wa bandari mpya ya Kibirizi

HALMASHAURI ya Manispaa ya Kigoma Ujiji huenda ikaingia kwenye kashfa na kushindwa kutekeleza azma yake ya kujenga bandari mpya ya Gati la Kibirizi kufuatia wananchi waliopisha ujenzi huo kulalamikia zoezi hilo kughubikwa na usiri mkubwa.

Zaidi ya vibanda 800 vya biashara na nyumba za makazi vitabomolewa ili kupisha ujenzi wa gati hilo unaojumuisha nchi tano zinazotumia ziwa Tanganyika lakini wananchi wameanza kuonyesha hofu na woga katika hatua za awali za kufanyiwa tathimini.

Wahanga wa eneo hilo wamefika kwenye ofisi ya kata ya Kibirizi ambapo baadhi ya wananchi waliofika baada ya kuitikia mwito wa viongozi wa Manispaa hiyo kupitia kwa mthamini wake  ili kujua  nini kinaendelea.

Wananchi hao wanapinga  kitendo cha mthamini wa Manispaa hiyo Steven Ambrose  kuwasainisha fomu zisizokuwa na kiwango cha malipo ya pesa wanazostahili.

Usiri huu unawafanya baadhi yao waamini kuwa huenda zoezi zima limeghubikwa na rushwa hali ambayo inasababisha kugawanyika  ambapo wengine wanakubali kusaini na wengine wakitaa huku Afisa Mtendaji wa Kata ya Kibirizi Alfan Mofu akijaribu kutetea uamuzi huo.

Hata hivyo mthamini wa Manispaa hiyo Steven Ambrose ambaye alikuwa eneo la tukio hakuwa tayari kulizungumzia suala hilo kwa madai kuwa yeye si msemaji.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kigoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa