Home » » Milioni 42 zatolewa kupunguza vifo vya Wajawazito wakati wa kujifungua Kigoma

Milioni 42 zatolewa kupunguza vifo vya Wajawazito wakati wa kujifungua Kigoma



ZAHANATI tatu za Misheni zilizopo Kata ya Kigoma Kaskazini Mkoani Kigoma  zimekabidhiwa Cheki ya Kiasi cha Tsh million 42 kwa lengo la kuwapatia huduma  ya kujifungua bure  akina  mama wajawazito ili kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi kwa kushindwa kugharamia huduma hiyo.

Fedha hizo zimekabidhiwa jana Kalinzi Mkoani humo na Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya kigoma vijijini, Bi. Miriam Mbaga kwa wawakilishi wa hospitali ya Matyazo, Bugabiro na Kiganza ambazo zote zinamilikiwa na makanisa ikiwa ni moja ya kampeni endelevu ya okoa maisha ya mama na mtoto ukanda wa kigoma kaskazini na mwambao wa ziwa Tanganyika.

Akikabidhi fedha hizo Mbaga aliwataka wanawake wa maeneo hayo wasiwe na hofu ya kufika kwenye zahanati hizo pindi wanapohisi wakati wa kujifungua umekaribia na kwamba serikali imesikia kilio chao cha gharama kubwa wanazopatiwa na hospitali hizo.

Aidha akiwataka kina baba kutoongeza  wake wengine kwa nafasi hyo badala yake waongeze upendo kwa wake zao kwenye ujauzito kwa kuwasindikiza kliniki ili kujua afya zao na kumlinda mtoto aliye tumboni.

Wakati huo huo Mbaya aliwataka wahudumu wa hospitali hizo kuachana na tabia za kuwanyanyasa wazazi pindi wawapo kwenye machungu ya kujifungua kwa kudai kuwa wengi wao hawana uelewa wa kutosh ahivyo watumie njia mbadala ya kuwaelimisha.

“wahudumu wa afya wa hospitali ya matyazo, bugabiro na kigaza tafadhali msiwanyanyase kwa kuwatukana wakati wengi wao wanauwelewa mdogo na mkumbuke uchungu ni nusu ya wazimu”. alisema Mbaga.

Kwa upande wake  Mganga Mkuu wa wilaya  Dkt. Edwin Kilimba alisema kuwa, wananchi pamoja na wahudumu wa halmashauri  watambue jitihada za mkurugenzi wa sasa zina lengo la dhati kwa kina mama kufuatia vifo ambavyo vimekua vikijitokeza katika wilaya yao.

Alisema baadhi ya viongozi wa halmashauri kuwakingia vifua waganga katika vituo vya afya vya serikali kwa kushindwa kutekeleza wajibu wao kwa wagonjwa ni tatizo linaleta utata katika kampeni ya okoa vifo vinavyoepukika kwa jamii husika.

Kwa upande wa kina mama wa kata ya Kalinzi walisema kuwa tukio hilo ni la kipekee tangu nchi ipate uhuru kwa kitendo cha mkurugenzi kuwa muwazi na mwenye lengo kwa wanawake wa kigoma, huku wakidai kuwa kufuatia huduma hiyo kutolewa bure hakuna mwanamke aliye tayari kuzalia nyumbani kwani uhakiaka wa huduma umewekwa wazi.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kigoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa