Home » » Wazalisha umeme kwa kutumia kelele, waunda jereta isiyotumia mafuta

Wazalisha umeme kwa kutumia kelele, waunda jereta isiyotumia mafuta

 

Emmanuel Ngowi akionyesha jenereta lisilotumia mafuta 

Mkufunzi wa ufundi Stadi kutoka Mamlaka ya Mafunzo ya Ufundi Stadi (Veta) Kigoma, Sirili Aloyce anasema kelele ni nyenzo muhimu inayoweza kuzalisha nishati ya umeme.Share


Wakati baadhi ya watu wakitumia njia mbalimbali kupambana na kelele za kila aina, wengine wanazitafuta ili waweze kufanya shughuli mbalimbali zenye matokeo chanya kwenye maisha ya binadamu.
Mkufunzi wa ufundi Stadi kutoka Mamlaka ya Mafunzo ya Ufundi Stadi (Veta) Kigoma, Sirili Aloyce anasema kelele ni nyenzo muhimu inayoweza kuzalisha nishati ya umeme.
Tayari Aloyce ameunda mashine inayotumia kelele na miyonzi ya mwanga kuzalisha nishati hiyo.
“Mashine hii hutumia kelele na mionzi ya mwanga kuzalisha umeme. Imeundwa na betri ya volti 12 kama kianzishio kisha huzalisha umeme wa volt 220 mpaka230. Umeme huo unaweza kuwasha balbu 10, televisheni na redio,” anasema Aloyce.
Akieleza jinsi mashine hiyo inavyofanya kazi, anasema imewekewa kinasa sauti (microphone) kinachopokea kelele zozote zile na kuzipeleka kwenye mitambo ya kuikuza kabla ya kuchanganyika na mionzi inayovutwa na kifaa maalum kisha kuchanganyika pamoja na kuchaji betri.
“Sauti na mionzi inayokusanywa wakati mashine imewashwa hukuzwa na kuingizwa kwenye mitambo ambayo hubadilishwa kuwa umeme,” anasema.
Aloyce anayesema kuwa, yeye ndiye mgunduzi wa teknolojia hiyo, anabainisha kuwa lengo lengo lake ni kuhakikisha kila mwananchi anaweza kupata nishati hiyo kwa njia rahisi.
Hata hivyo anasema bado anaendelea na utafiti wake ili mashine hiyo izalishe umeme mkubwa zaidi.
“Nia yangu ni kuhakikisha kuwa umeme huu unasaidia watu nyumbani na matumizi ya viwandani,” anasema na kuongeza:
“Hadi sasa nimetumia Sh800,000 kuunda mashine hii, hatua iliyobaki ya kuhakikisha inazalisha umeme mkubwa zaidi. Haitachukua muda mrefu kwa sababu kazi iliyobaki siyo kubwa sana. Lengo langu ni kuifanya izalishe umeme wa wati 6000 na kuifanya kuwa ya kisasa zaidi.”
Jenereta ya kuzalisha umeme bila kutumia mafuta
Mbali na teknolojia hiyo ya kuzalisha umeme kwa kutumia mawimbi ya sauti mbalimbali, mwanafunzi wa chuo hicho naye ametegeneza jenereta inayoweza kuzalisha umeme bila kutumia mafuta.





CHANZO MWANANCHI  GAZETI

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kigoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa