Home » » Mhasibu auawa na kuporwa fedha

Mhasibu auawa na kuporwa fedha



MHASIBU wa kampuni ya pamba ameuawa kwa kupigwa risasi kichwani na kisha kuporwa zaidi ya shilingi milioni nane wilayani Igunga.

Kamanda wa Polisi Mkoani Tabora kamishna msaidizi wa Polisi Peter Ouma, alisema tukio hilo limetokea Wilayani Igunga usiku wa kuamkia jana na kumtaja marehemu kuwa ni Agnes Aron (44) aliyegiwa risasi ya kichwani na watu wanaodhaniwa ni majambazi waliovamia kwenye ghala la pamba alilokuwepo.

Akizungumzia tukio hilo, Kamanda Ouma amesema watu watatu walivamia ghala la pamba katika kijiji cha Iyogelo,kata ya kining'inila,wilayani igunga majira ya saa mbili usiku na kumpiga risasi kichwani mhasibu huyo kwa kutumia gobole.

Baada ya kumuua walimpekua na kuchukua kiasi ambacho inakisiwa ni zaidi ya shilingi Milioni nane alizokuwa nazo mhasibu huyo ndani ya ghala hilo.

Ameeleza kuwa mhasibu huyo na wenzake walikuwa ndani ya ghala wakipokea pamba na kupakia kwenye malori na ndipo walipovamiwa.

Hata hivyo amesema tayari polisi inamshikilia mtu mmoja ambaye jina lake limehifadhiwa kuhusiana na tukio hilo huku akitoa wito kwa makampuni ya pamba kutumia walinzi katika shughuli zao.

kamanda Ouma aliongeza kuwa atakuwa na mazungumzo na makampuni ya pamba ili kuwasisitiza umuhimu wa kuwa na ulinzi katika shughuli zao huku akionya kutotembea na pesa nyingi hadi usiku.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kigoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa