Home » » Vyama vya siasa vyatia doa uchaguzi wa makamo mwenyekiti Kigoma

Vyama vya siasa vyatia doa uchaguzi wa makamo mwenyekiti Kigoma



UCHAGUZI wa Makamu Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma na wenyeviti wa kamati mbalimbali za baraza la madiwani wa halmashauri hiyo nusra uvunjike baada ya kutawaliwa na hisia za vyama kati ya Chama cha Mapinduzi CCM na NCCR Mageuzi.
Mvutano huo ulitokana na kulingana kwa idadi ya wajumbe kati ya vyama vyote viwili huku chama cha Wananchi CUF chenye diwani mmoja wa viti maalumu kikiwa kivutio ambapo kura yake ilitakiwa na kila chama ili kishinde na hatimaye NCCR Mageuzi kiliibuka na ushindi wa kura 21 dhidi ya kura 20 za CCM.

Hatua iliyolalamikiwa na baadhi ya madiwani ni kitendo cha Mwenyekiti wa halmashauri ambaye anatoka CCM kuketi kitako na timu ya wataalamu akiwemo Mkurugenzi Mtendaji ili kuwapangia kamati wajumbe bila ridhaa yao hatua ambayo iliwakasirisha na kupinga uamuzi huo.

 Kikao hicho kutawaliwa na hisia za kivyama kulisababisha ajenda nyingine kuchelewa kujadiliwa huku wengine wakirushiana maneno ya kuwalaumu wabunge kuwa wazungumzaji kuliko madiwani.

Wilaya ya Kasulu kabla ya kugawanywa na kupatikana kwa wilaya mpya ya Buhigwe ilikuwa na majimbo mawili ya uchaguzi yanayoongozwa na wabunge Agripina Buyogera na Moses Machali wote kutoka chama NCCR Mageuzi huku huku diwani wa Kata ya Kasulu mjini akiiongzea nguvu baada ya kuibuka mshindi katika nafasi ya makamu mwenyekiti wa halmashauri hiyo.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kigoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa