Na Diana Rubanguka, Kigoma.
MKANDARASI
wa kampuni ya ILAGA JONTA iliyopo mkoani Kigoma ameshindwa kukabidhi mradi wa
soko la Mgaraganza lililopo katika Kijiji cha Mgaraganza Mkoani
humo kutokana na ujenzi wa soko hilo kuwa chini ya kiwango.
Akizungumza na
waandishi wa habari katika kijiji hicho Mwenyekiti wa Kijiji bw Yunusi Shabani
alisema kuwa mkandarasi huyo ambaye alianza ujenzi wa soko hilo tangu Mai, 2010
na kutakiwa kukabidhi Septemba, 2010 ambapo ameshindwa kufanya hivyo kutokana
na soko hilo kuto kuwa na ubora unaotakiwa.
Bw. Shabani alisema
kuwa ujenzi huo umechukua taakribani miaka miwili kutokana wakaguzi
kutokuridhishwa na ujenzi huo ambao upo chini ya viwango na hivyo mkandarasi
huyo kulazimika kufanya ukarabati wa mara kwa mara katika sokohilo.
Aidha mradi huo wenye thamani ya shilingi milioni 28 ambao upo chini ya serikali kupitia Dasp pamoja na nguvu za wananchi wa kijiji hicho bado haujakabidhiwa kwa wananchi kutokana na mapungufu hayo jambo ambalo limekuwa kero kwa wananchi wa kijiji hicho na kuitaka serikali kumchukulia hatua za kisheria kwa mkandarasi huyo kutokana na kukiuka mkataba wake.
Aidha mradi huo wenye thamani ya shilingi milioni 28 ambao upo chini ya serikali kupitia Dasp pamoja na nguvu za wananchi wa kijiji hicho bado haujakabidhiwa kwa wananchi kutokana na mapungufu hayo jambo ambalo limekuwa kero kwa wananchi wa kijiji hicho na kuitaka serikali kumchukulia hatua za kisheria kwa mkandarasi huyo kutokana na kukiuka mkataba wake.
Hata
hivyo juhudi za kuwasiliana na mkandarasi zinaendelea ili kujua ni lini
atakabidhi mradi huo kwa wananchi ili waweze kunufaika na mradi huo ambao
wamechangia nguvu zao kwa asilimia 20 katika kuhakikisha mradi wa soko hilo
unakamilika kwa wakati uliopangwa.
0 comments:
Post a Comment