Home » » KATA 14 KUWANIA KAFULILA CUP

KATA 14 KUWANIA KAFULILA CUP

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

WAKATI akiendelea na Kampeni ya ‘Rudisheni Pesa Zetu’, inayoshika kasi mkoani Kigoma, Mbunge wa Kigoma Kusini (NCCR-Mageuzi), Thomas Kafulila, ametangaza kuanza kwa michuano ya kuwania ng’ombe sita itakayoshirikisha timu za kata zinazounda jimbo hilo.
Akizungumza katika Kijiji cha Basanza, Kata ya Uvinza kwenye mfululizo wa mikutano yake ya kampeni hiyo, Kafulila alizitaja kata zitakazoshiriki michuano hiyo kuwa ni Uvinza, Nguruka, Sigunga, Ilagala, Simbo, Sunuka, Kazuramimba, Kalya, Bulungu, Igalula, Mtego wa Noti, Kandaga, Itebula na Mganza.
Alibainisha kuwa kila timu katika michuano hiyo itapewa jezi na mpira, ili kujiandaa ambapo bingwa atajinyakulia zawadi ya ng’ombe watatu, wakati mshindi wa pili akibeba ng’ombe wawili na mshindi wa tatu akitoka na ng’ombe mmoja.
Aliwataka wachezaji wa timu shiriki kukubali matokeo katika michuano hiyo, kwani kufunga na kufungwa ni kitu cha kawaida katika soka, kama ilivyoonekana kwenye fainali za Kombe la Dunia nchini Brazil, ambako wenyeji licha ya ubora na umwamba wao duniani, walikubali kipigo cha mabao 7-1 kutoka kwa Ujerumani.
Kafulila alisema kuwa lengo la michuano hiyo ni kuhamasisha meandeleo ya michezo katika jimbo hilo, huku akijipanga kuratibu pia michuano ya soka la wanawake
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kigoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa