Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
MENEJA wa Mfuko wa  Bima ya afya Mkoa wa Kigoma (NHIF), Elias 
Odhiambo amewataka waandishi wa  habari mkoani hapa kujiunga na bima ya 
afya ili kuondokana na hofu ya kukosa  matibabu wanapoumwa.
  Akizungumza na  Waandishi wa Habari katika ofisi za Chama cha 
Waandishi wa Habari Mkoa wa  Kigoma (KGPC), Meneja huyo alisema kuwa, 
gharama ya kujiunga na mfuko huo kwa  vikundi au taasisi isiyo ya 
serikali ni sh 76,300 kwa kila mwanachama, ambako  atapata matibabu kwa 
mwaka mzima kwa fedha hiyo.
  ”Hivi sasa gharama  za matibabu kwa kweli zipo juu sana, hivyo ni 
wakati wa kuangalia mnaelekea  wapi, kujiunga na bima ya afya ni suala 
la msingi ili kuwa na uhakika wa  matibabu unapougua, kwani unaweza 
kuugua kipindi ambacho huna hata pesa  mfukoni, mtafakari vizuri na 
kufanya maamuzi,” alisema Odhiambo.
  Meneja huyo  alisema, huduma zinazotolewa na NHIF ni bora zaidi, kwani
 zinampa mwanachama  uhuru wa kuchagua mahali au kituo anachopenda 
kupata huduma ya matibabu.
  Alisema, hadi sasa  NHIF imesajili vituo vya afya na maduka ya dawa 
5,840 kwa nchi nzima, hali  inayorahisisha upatikanaji wa huduma kwa 
wananchama.
  Naye Mwenyekiti wa  KGPC, Deogratius Nsokolo, alisema, wanachama wake 
watajiunga na mfuko huo kwa  kuwa una manufaa makubwa na wataishawishi 
jamii kujiunga na mfuko huo.
Chanzo:Tanzania Daima 
0 comments:
Post a Comment