Home » » DKT. NDUGULILE ASHIRIKI UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI YA KIJIJI CHA NYANGANGA KATIKA ZOEZI LA KUAMSHA ARI YA WANANCHI KUCHANGIA SHUGHULI ZA MAENDELEO MKOANI KIGOMA

DKT. NDUGULILE ASHIRIKI UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI YA KIJIJI CHA NYANGANGA KATIKA ZOEZI LA KUAMSHA ARI YA WANANCHI KUCHANGIA SHUGHULI ZA MAENDELEO MKOANI KIGOMA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile(Mb) akishirikiana na wananchi wa Kijiji cha Nyanganga kuchanganya zege kwa ajili ya kuweka ‘rental’ kwa ajili ya madarasa manne ya Shule ya Kijiji hicho katika zoezi la kuamsha ari ya wananchi kujitolea katika kufanya shughuli za maendeleo.
Mtendaji wa Kjjiji cha Nyanganga Bw.Erick Ruhomola akitoa taarifa ya Mradi wa ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Kijiji chao kwa Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile(Mb) ambao uliibuliwa, kubainishwa na kutekelezwa wananchi wenyewe na wananchi kwa takribani.
Mkuu wa Wilaya ya Uvinza Mhe. Mwanamvua Mrindiko akimshukuru Naibu Waziri Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile(Mb) kwa kuja kuonesha mfano wa kuamsha ari ya wananchi wa Uvinza kujitolea katika shughuli za maendeleo yao.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile(Mb) akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Nyanganga mara baada ya kushiriki zoezi la kuamsha ari katika ujenzi wa Shule ya Kijiji hicho.
Wananchi wa Kijiji cha Nyanganga wakimsikiliza Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile(Mb) mara baaada ya kushirikiana naye katika zoezi la kuamsha ari ya wananchi kufanya kazi katika ujenzi wa vyumba vine vya madarasa ya shule ya Sekondari ya Kijiji chao.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile(Mb) akikabidhi mifuko 37 ya Saruji kwa ajili ya kuunga mkono juhudi za wananchi wa Kijiji cha Nyanganga wa kujitolea kwa nguvu zao kujenga shule ya Sekondari ya Kijiji chao.
Baadhi ya wananchi wakifanya kazi ya kumwaga ‘rental’ katika ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Kijiji cha Nyanganga kilichopo Wilaya ya Uvinza Mkoani Kigoma.Picha zote na Kitengo cha Mawasiliano WAMJW

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile(Mb) akitia saini katika kitabu cha wageni mara alipowasili katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma kwa ajili ya Ziara ya siku mbili ya kikazi Mkoani hapo.




Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Kigoma Dkt. Paul Chaote akitoa taarifa ya Mkoa kwa Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile(Mb) katika Ziara ya siku mbili ya kikazi ya Naibu Waziri huyo Mkoani hapo.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile(Mb) akisalimiana na wananchi wa Kijiji cha Nyanganga mara baada ya kuwasili katika kushiriki ujenzi wa madarasa manne ya Shule ya Kijiji hicho katika kuamsha ari ya wananchi kujitolea katika kufanya shughuli za maendeleo.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya Uvinza Bw. Lutabola Weja akitoa ufafanuzi wa jambo wakati wa zoezi la kuamsha ari ya wananchi kujishughulisha katika shughuli za maendeleo ambapo wanachi wa Kijiji cha Nyanganga wamejitolea na kujenga vyumba vinne vya madarasa kwa ajili ya shule ya Kijiji chao.


Na Kitengo cha Mawasiliano WAMJW

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile(Mb) ameshiriki ujenzi wa Shule ya Kijiji cha Nyanganga iliyoko kata ya Kazuramimba, wilaya ya Uvinza mkoani Kigoma ikiwa ni jitihada za wananchi wa kijiji hicho kuharakisha upatikanaji wa huduma ya elimu kijijini hapo.

Akiwa katika Kijiji hicho Naibu Waziri Dkt. Ndugulile ameshiriki zoezi la kumimina zege kwa ajili ya kufunga ‘rental’ ya vyumba vya madarasa ya shule hiyo.

Dkt. Ndugulile amesema lengo la kuwepo ziara hiyo ni kufuatilia utekelezaji wa Sera ya Maendeleo ya Jamii (1996), na Sera nyingine za Wizara amabzo zinasisitiza ushiriki wa jamii katika kuibua mahitaji, kupanga, kuamua, kutekeleza, kufuatilia na utathmini shughuli za miradi ya maendeleo ikiwemo uboreshaji wa huduma ya miundo mbinu ya kufundishia na kujifunzia katika maeneo ya mijini na vijijini.

Mhe. Ndugulile ameongeza kuwa Ili kurejesha ari ya wananchi kushiriki katika maendeleo yao kuelekea uchumi wa kati na wa viwanda, Wizara imeamua kufuatilia utekelezaji wa Sera ya Maendeleo ya Jamii katika ngazi za Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa kuhamasisha jamii kushiriki na kuchangia shughuli za maendeleo yao kwa kufanya kazi za bega kwa bega, kuchangia nguvu zao, rasilimali fedha, rasilimali vifaa na ufundi kwenye utekelezaji wa miradi ya ujenzi wa miundo ya elimu, afya, kilimo, mifugo, barabara na viwanda vidogo vidogo. 

“Nimeambiwa kuwa mradi wenu wa ujenzi wa shule ya sekondari katika kijiji cha Nyanganga utasaidia kusogeza huduma ya elimu jirani na wananchi, na nimevutiwa na hamasa mliyonayo katika maendeleo name nimekuja kushirikiana nanyi kuendeleza ujenzi wa madarasa ya shule kazi amabyo ni kigezo thabiti cha cha dhamira ya dhati yawananachi wa kijiji hiki katika kutoa haki ya msingi ya kumwendeleza Mtoto katika ngazi ya kijiji na jamii kwa ujumla” alisisitiza Mhe. Dkt. Ndugulile.

Kwa upande wake Mtendaji wa Kjjiji cha Nyanganga Bw.Erick Ruhomola amesema kuwa Mradi wa ujenzi wa Shule ya Sekondari ya kijiji uliibuliwa na kubainishwa na wananchi wenyewe na kutekelezwa na wananchi kwa takribani asilimia mia moja hadi kufikia hatua ya kumwaga zege kwa ajili ya ‘rental’.

“Tunaishukuru Serikali kwa kutuona na kuja kutuunga mkono katika jitihada zetu za kujiletea maendeleo katika kijiji chetu” alisisitiza Bw. Ruhomola.Naye Mkuu wa Wilaya yaUvinza Mhe. Mwanamvua Mrindiko amemshukuru Naibu Waziri kwa kuja kuonesha mfano wa kuamsha ari ya wananchi wa Uvinza kujitolea katika shughuli za maendeleo yao.

“ Hili ni Jambo la kipekee kwa Mhe. Naibu Waziri kutembelea na kushiriki na wananchi katika ujenzi wa shule hii” alisisitiza Mhe.Mwnanamvua

Ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Kijiji cha Nyanganga kilichopo Wilaya ya Uvinza Mkoa wa Kigoma itawasaidia watoto wa jamii hiyo kuwa na shule karibu na makazi yao ambapo hapo awali watoto hao walikuwa wanatembea umbali wa kilometa 14 kwenda shule ya jirani.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile yupo katika Mkoa wa Kigoma kwa ziara ya siku mbili ya kikazi kufuatilia utekelezaji wa Sera mbalimbali zinazosimamiwa na Wizara yake.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kigoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa