KAMATI ZA MAAFA HALMASHAURI YA KIGOMA UJIJI ZAPATIWA MAFUNZO YA KUKABILIANA NA MAAFA

Na Mwandishi wetu,KIGOMA.Maafisa wa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu (Idara ya Menejimenti ya Maafa) kwa kushirikiana na Shirika la Kimataifa linaloshughulikia uhamaji (IOM) wameendesha semina ya kujenga uelewa juu ya upunguzaji wa madhara ya maafa katika jamii.Mafunzo hayo yamefanyika tarehe 25 Machi 2025 katika Manispaa ya Kigoma Ujiji ambapo yamehudhuriwa na washiriki 50 ikiwemo Watendaji wa Kata, Watendaji wa Vijiji, Watendaji wa Mtaa Kamati za Maafa za Kata na Vijiji pamoja na mtaa.Akizungumza wakati wa ufunguzi wa semina hiyo kwa niaba ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma Ujiji Bi.Petronila...

BASHE ASEMA RAIS SAMIA HATAKI UTANI KILIMO CHA UMWAGILIAJI

WAZIRI wa Kilimo Hussein Bashe amewahakikishia Watanzania kuwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan amedhamiria kuleta mapinduzi sekta ya Umwagiliaji, hivyo miradi yote aliyoahidi itatekelezwa.Waziri Bashe amesisitiza utekelezaji wa miradi hiyo unaofanywa na Tume ya Taifa ya Umwagiliaji si hadithi bali umelenga  kuinua sekta ya Kilimo cha Umwagiliaji na kuchochea ukuaji wa uchumi nchini.Ameitakata Tume ya Taifa ya Umwagiliaji kujipanga kuhakikisha wanatekeleza miradi hiyo na wananchi wapuuze wanaowalaghai kuuza mashamba.Waziri Bashe amesema hayo Wakati akizungumza na wadau wa umwagiliaji katika eneo la mradi wa Luiche, ambapo amemshukuru...

DULLA MAKABILA, LINEX WAPAMBA TAMASHA LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

Mkali wa Singeli Abdallah Ahmed maarufu Dulla Makabila akiwa jukwaani kutumbuiza katika tamasha hilo la burudani kuelekea uzinduzi wa Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura mkoani Kigoma. Wasanii wa muziki wa Bongo Fleva na Singeli,  Sande Mangu almaarufu Linex na Abdallah Ahmed maarufu Dulla Makabila leo Julai 18,2024  wameingiza shangwe kwa wakazi wa Kigoma kwa kutoa burudani kali katika Tamasha la uzinduzi wa Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura. Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) inataraji juzindua Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Mpiga Kura Julai 20, 2024 utakaofanyika katika Uwanja wa...

PINDA AMREJESHEA NYUMBA BIBI ALIYOIHANGAIKIA KWA ZAIDI YA MIAKA 10 KIGOMA

 Na Munir Shemweta, Kigoma Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Geophrey Pinda amemrejeshea nyumba Bi Leticia Benedict Choma mwenye umri wa zaidi ya miaka 80 mkazi wa Kigoma Ujiji baada ya kuihangaikia kwa zaidi ya miaka 10 bila mafanikio. Bi. Leticia Choma anadaiwa kudhulumiwa nyumba aliyoachiwa na marehemu baba yake Bw. Benedict Choma iliyopo eneo la Mwanga barabara ya Bibi Titi Kigoma Ujiji kama urithi baada ya nyumba hiyo kuuzwa na msimamizi bandia wa mirathi asiyeidhinishwa na mahakama kwa madai ya kutokuwa na haki ya kumiliki nyumba hiyo licha ya  wazazi wake kujenga na yeye kuzaliwa na kuishi...

ZIARA YA MAKAMU WA RAIS BUHIGWE NA KIGOMA VIJIJINI

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Kalinzi akiwa ziarani Mkoa wa Kigoma tarehe 09 Julai 2024.&nb...

MWALIM MKUU KAKONKO AJINYONGA AKIWA OFISINI KWAKE,AANDIKA UJUMBE UNAOMUHUSU MKURUGENZI.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. MKUU wa Shule ya Sekondari Kakonko wilayani Kakonko mkoani Kigoma,Peter Rubonya amefariki dunia baada ya kujinyonga kwa kamba ofisini kwake mapema leo asubuhi.Akielezea tukio hilo,Mwalim wa zamu wa shule hiyo Isaac Japhet amesema yeye alifika shuleni hapo saa 12:30 asubuhi ili kuwafundisha wanafunzi wa kidato cha nne masomo ya ziada baada ya kufunga shule wiki iliyopita na baada ya kufika aligundua kuwa hana chaki ambapo mkuu huyo wa shule alimpatia chaki mlinzi ili awape wananfunzi.Amesema baada ya muda,Mratibu...

WATU SABA WAFARIKI AJALI YA LORI KIGOMA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. Na Rhoda Ezekiel- Malunde1 blog Watu saba wamefariki dunia katika ajali ya gari aina ya Scania katika  Mlima wa Kasagamba kijiji cha Mkongoro barabara ya kutoka Manyovu wilaya ya Kigoma Vijijini kuelekea mkoani Kigoma. Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoani Kigoma Maltini Otieno amesema ajali hiyo imetokea leo Machi 21, 2018 majira ya saa tatu asubuhi.  Amesema gari aina ya Scania lori yenye namba T741 AAB  ilianguka na kusababisha vifo vya watu saba akiwemo dereva wa gari hiyo...

ULEGA AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA KWA MKAKATI MZURI WA KUINUA SEKTA YA MIFUGO NA UVUVI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.  Chaga za kisasa za kukaushia dagaa katika mwalo wa Muyobozi, uliyopo katika kijiji cha Mwakizega Wilayani Uvinza, Mwalo ambao ulijengwa na Mradi wa kuhifadhi mazingira ya ziwa Victoria LIVEMP , chaga hizo zinatumika na wavuvi kukaushia dagaa.  Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdalah Ulega na Ujumbe wake wakitoka kukagua gati katika mwalwo wa Muyobozi uliyopo Wilayani uvinza katika kijiji cha Mwakizega ambapo Naibu Waziri Ulega alifanya ziara leo. Afisa Uvuvi wa Wilaya ya Uvinza Bw. Haroon...
 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kigoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa