
Na Mwandishi wetu,KIGOMA.Maafisa wa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu (Idara ya Menejimenti ya Maafa) kwa kushirikiana na Shirika la Kimataifa linaloshughulikia uhamaji (IOM) wameendesha semina ya kujenga uelewa juu ya upunguzaji wa madhara ya maafa katika jamii.Mafunzo hayo yamefanyika tarehe 25 Machi 2025 katika Manispaa ya Kigoma Ujiji ambapo yamehudhuriwa na washiriki 50 ikiwemo Watendaji wa Kata, Watendaji wa Vijiji, Watendaji wa Mtaa Kamati za Maafa za Kata na Vijiji pamoja na mtaa.Akizungumza wakati wa ufunguzi wa semina hiyo kwa niaba ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma Ujiji Bi.Petronila...