Home » » EXIM YAZINDUA TAWI

EXIM YAZINDUA TAWI



na Mwandishi wetu, Kigoma
BENKI ya Exim imeendelea kupanua huduma zake nchini kwa kuzindua tawi jipya mkoani Kigoma, ikiwa ni jitihada za kuwafikishia huduma za kibenki wananchi wengi zaidi nchini.
Tawi hilo jipya litakuwa la 23 nchi nzima huku benki hiyo ikiwa imethubutu kufungua matawi mengine mawili nje ya nchi yakiwa nchini Comoro na Djibouti.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa tawi hilo, Mkurugenzi wa benki hiyo, Hanif Jaffer, alisema ufunguzi wa tawi hilo ni utekelezaji wa mpango wa benki unaolenga kuhakikishia wananchi wengi wanapata huduma bora za kibenki.
Jaffer alisema benki yake imeamua kufungua tawi hilo kutokana na ukweli kuwa Mkoa wa Kigoma ni kiungo muhimu kwa wananchi wanaofanya biashara na nchi jirani za Burundi na Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo.
Alisema kuwa benki yake itaendelea kuwapatia wajasiriamali wadogo na wakati uwezo wa kifedha ili kuwasaidia kupanua biashara zao.
“Jitihada zetu ni kuhakikisha tunafikia wananchi wengi waliopo pembezoni. Tuna imani kuwa ufunguzi wa tawi letu jipya hapa litasaidia kupunguza tatizo hilo,” alisema Jaffer.
Chanzo: Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kigoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa