Home » » Mbwa 900 wapatiwa chanjo ya kuzuia ugonjwa wa kichaa Kigoma

Mbwa 900 wapatiwa chanjo ya kuzuia ugonjwa wa kichaa Kigoma

ILI kukabiliana na ongezeko la ugonjwa wa kichaa cha mbwa unaowakabili baadhi ya wananchi mara baada ya kushambuliwa na Mbwa mwenye ugonjwa huo halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji imeendesha zoezi maalum la kuwachanja mbwa wapatao 900 ili kuepusha madhara kwa binadamu.

Zoezi hilo linafanyika kwa mara ya kwanza mkoani humo kwa ushirikiano wa mashirika mbalimbali ambayo ni pamoja na hifadhi za taifa ya Gombe, mradi wa magonjwa ya wanyama Serengeti, taasisi ya Jane Goodall na Manispaa hiyo.

Takwimu za shirika la Afya ulimwenguni WHO linaonyesha kuwa watu 55,000 wanapoteza maisha kwa mwaka sawa na wastani wa kifo kimoja kila baada ya dakika 10 hususani kwenye nchi za Asaia na Afrika chini ya Jangwa la Sahara ikiwemo Tanzania.
 Dr. John Shauri ni Daktari wa wanyama katika halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji ambaye amesema kuwa Kwa mujibu wa takwimu hizo wanaopata madhara zaidi ni watoto kutokana na tabia yao kupenda kucheza na wanyama  ambao hushambuliwa zaidi kichwani, usoni au shingo maeneo ambayo ni hatari kwa ugonjwa wa kichaa cha mbwa.

Kwa upande wake mratibu wa zoezi hilo Dr. Iddi Lipende amesema watu wazima nao hupata ugonjwa ambapo aslimia 99.9 ya wagonjwa walioonyesha dalili za ugonjwa huo hufariki dunia kutokana na kutowahi mapema ili kupata tiba

Ameongeza kuwa Mara baada ya kumalizika kwa zoezi hili wamiliki wa mbwa watalazimika kulipia kiasi cha sh 5,000 ili kupata huduma lakini kwa waliobahatika kufika eneo la tukio na kupata chanjo wanaelezea kufurahishwa kwao na zoezi jinsi lilivyoendeshwa.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kigoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa