Home » » Waziri Mkuu Mizengo Pinda aanza ziara ya siku saba Mkoani Kigoma

Waziri Mkuu Mizengo Pinda aanza ziara ya siku saba Mkoani Kigoma

Na Diana Rubanguka, Kigoma.

Waziri Mkuu Mizengo Pinda anatarajia kuwasili leo mkoani Kigoma kwa lengo la kufanya ziara ya kikazi itakayochukua takribani muda wa siku saba.

Taarifa toka ofisi ya mkuu wa mkoa wa Kigoma Kanal Mstaafu Issa Machibya kwa waandishi wa habari mkoani humo imesema waziri Pinda anatarajia kuwasili leo majira ya saa tano asubuhi kwa usafiri wa Ndege.

Katika ziara hiyo atafanya shughuli muhimu ambapo miongoni mwa shughuli hizo ni pamoja na taarifa ya maendeleo ya mkoa huo na kuona siraha zilizokamatwa wakati wa operation katika kituo kikuu cha polisi mkoani kigoma.

Pia atafanya uzinduzi katika ofisi za wilaya ya Kakonko, Buhigwe, uvinza pamoja na  chuo cha kilimo Mubondo, sanjari na kuweka jiwe la msingi katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri ya Uvinza  pamoja na bank  ya NMB.

Aidha atatembelea miradi mbalimbali Mkoani kigoma ikiwemo ufugaji wa nyuki pamoja na bwawa la umwagiliaji Nyendara pamoja na kukagua hifadhi ya situ wa ufugaji nyuki.

Mheshimiwa pinda atatembelea vikundi mbalimbali vya ujasiliamali pamoja na kufanya mikutano ya hadhara katika maeneo mbalimbali mkoani humo .

Katika ziara hiyo  mheshimiwa pinda atatembelea pia wilaya sita zilizopo mkoani kigoma  ambazo ni Wilaya ya Uvinza ambayao imetokana na Wilaya ya Kigoma, Wilaya ya Buhigwe ambayo imetokana na Wilaya ya Kasulu, pamoja na Wilaya ya Kakonko ambyo imetokana na Wilaya ya Kibondo. 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kigoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa