Home » » Timu ya Katubuka yaibuka bingwa ligi ya wiki ya nenda kwa usalama

Timu ya Katubuka yaibuka bingwa ligi ya wiki ya nenda kwa usalama

Na Diana Rubanguka, Kigoma
TIMU ya Mpira wa pete ya Shule ya Sekondari ya Katubuka iliyopo katika Manispaa ya Kigoma ujiji imejinyakulia kitita cha sh.500,000 baada ya kutwaa ubingwa wa ligi  ya Wiki ya Usalama Barabarani  ikiwa na lengo la kuhamasisha wadau wake wazingatie sheria na kanuni za  Barabara.

Hayo yamebainika jana Mkoani Kigoma  wakati Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama barabarani  mkoani hapa, Abdulqadir Mushi alipokuwa akitaja timu zilizoshiriki na kufanikiwa kuingia nusu fainali na washindi wa ligi hiyo ambapo timu ya buhanda ikipata kifuta jasho cha sh.200,000 baada ya kushika nafasi ya pili.

Kwa upande wa Mwenyekiti wa Chaneta Mkoa wa Kigoma  Amina Malengwa alisema  timu zimeonesha uwezo wao kimashindano katika dakika zote 60,ambapo timu ya mpira wa pete  sekondari ya katubuka iliibuka kwa vikapu 25-21 dhidi ya sekondari ya Buhanda.

Kwa upande wa walimu wa timu ya sekondari Katubuka Joanita Emanueli na Siyaleo Sadock mwalimu wa sekondari Buhanda kwa nyakati tofauti walikiri timu zote kucheza vizuri huku waonya mashindano kama hayo viongozi watoe tarifa za ushiriki kwa timu husika mapema ili wajiandae vyema na zawadi ziongezwe.

Kwa nyakati tofauti wachezaji wa ligi hiyo sekondari ya katubuka Hawa Abdalla  na Nuru Himid walidai timu ya Buhanda ilibebwa na mwamuzi aliyechezesha ligi hiyo Wakati Bernadeta Bernad Sekondari Buhanda alidai wachezaji wa timu ya sekondari ya katubuka walikuwa wababe katika ukabaji na kuahidi mwakani watatoa kipigo cha magori dhidi ya timu hiyo inayoogopwa katika manispaa ya ujiji.

Jambo Leo imebaini changamoto inayowafanya wachezaji wa timu za mpira wa pete kutosonga mbele inatokana na urasimu unaofanywa na viongozi wa serikali kutoweka umuhimu katika sekta hiyo kwa madai haina  bajeti yake mbaya zaidi hakuna jitihada za kuwekea bajeti hatimaye wachezaji wakosa ajira kupitia michezo.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kigoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa