KATIKA kukabiliana na hali
ngumu kichumi Klabu ya waandishi wa habari mkoani Kigoma KGPC imejiunga na
mfuko wa hifadhi ya Jamii wa LAPF ili kuwawezesha wanachama wake kujitegemea
badala ya kuvitegemea vyombo vya habari ambavyo hata hivyo huwalipa maslahi
duni.
Hatua hiyo inatajwa
kuwa mkombozi kwa waandishi hao ambao wamekuwa tegemezi kwa muda mrefu licha ya
kufanya kazi katika mazingira magumu na hatarishi lakini pindi wanapopata
matatizo ya kifamilia hukosa mahali pa kukimbilia.
Umoja wa vilabu vya
habari nchini UTPC ukiwa ndio nguzo pekee ya kuwalea wanahabari hususani
wanaoishi mikoani umeshiriki kwa karibu katika kuviunganisha vilabu vya habari
hapa nchini na sekta mbalimbali za kifedha ili kuhakikisha mwanataaluma ya
habari anaondokana na umasikini wa kipato.
Makamu wa Rais wa
UTPC Bi. Jane Mihanji amesema umoja huo umekuwa ukitafuta njia mbadala ambazo
zitasaidia kuwapunguzia wanahabari ukali wa maisha ambapo sasa imekuja na mbinu
mpya ya kuanzisha chama cha kutetea maslahi ya waandishi.
Mwenyekiti wa KGPC
Deo Nsonkolo amesema ni Klabu ya kwanza nchini kujiunga na mfuko huo, KGPC
imedhamiria kuwakomboa wanachama wake kutoka kwenye lindi la umasikini ambapo
inakadiriwa kuwa asilimia 80 ya waandishi wa habari mkoani humu hawana ajira za
kudumu kutoka kwenye vyombo wanavyofanyia kazi.
0 comments:
Post a Comment