Home » » POLISI WAMNASA MUUGUZI KWA WIZI WA DAWA ZA SERIKALI MKOANI KIGOMA

POLISI WAMNASA MUUGUZI KWA WIZI WA DAWA ZA SERIKALI MKOANI KIGOMA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Jeshi la Polisi Mkoani Kigoma linawashikilia wakazi wawili wa kijiji cha Kaguruka kata ya Rungwe Mpya wilayani Kasulu akiwemo muuguzi wa zahanati ya kijiji hicho wakituhumiwa kuiba dawa za serikali zilizoletwa katika zahanati hiyo.

Kamanda wa polisi Mkoa wa Kigoma Kamishna msaidizi mwandamizi wa polisi FERDINAND MTUI amesema watu hao ambao majina yao yamehifadhi , walishtukiwa na wananchi baada ya muuguzi huyo kuiba na kumkabidhi mwananchi mwingine kwa lengo la kuficha.

Hata hivyo wananchi walibaini wizi huo na kuanza kuwashambulia mpaka viongozi wa kijiji walipofika na kuwafungia watuhumiwa ofisi ya kijiji ili kunusuru maisha yao.


Kamanda MTUI amesema watuhumiwa hao walikuwa wameiba dawa za aina mbalimbali za binadamu na vipimo vya malaria ambavyo thamani yake haijafahamika na kwamba watafikishwa mahakamani.
 
CHANZO VIJIMAMBO BLOG

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kigoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa